Michael Mkwanzania
Member
- Jun 8, 2016
- 83
- 652
Jiji la dar-es-salaam limejaa vivuli vya kutafuta kwangu na vya watu wengi sana. Kila mtaa ninaopita naviona, najiona mwenyewe nilivyokua natembea hii mitaa, Kugonga milango kwenye ofisi za wahindi na kuwaelezea nini nachoweza fanya, kugonga milango hiyohiyo tena na kuambiwa nirudi wiki ijayo ili kupata malipo, wakati sijui hata jioni hiyo nitakula vipi, kugonga milango na kukutana na middle men ambao wanataka hela kidogo kabla hawajakuonganisha kwa bosi, au percent ya proposal kama ikipita.
Vivuli vya zaidi ya miaka kumi ya kutafuta na kuto kubali kushindwa, vivuli vya huu mji aisee.
Vivuli vya marafiki tuliyoenda njia tofauti, vivuli vya watu uliyodhani ni marafiki, vivuli vya december na njaanuary ambapo jua linapiga hadi kero, lakini bado tunatembea na kutafuta, maana hamna njia nyingine ukiwa mtafutaji.
Hapo kati vikaja vivuli vyenye kutia moyo kidogo, kivuli cha mara ya kwanza kushika milioni moja shilingi, aisee niliona hamna kitu kinashindikana. Nikakodi chumba cha pili kuweza expand mishe, nkasema kama milioni nmeiweza kwanini nishindwe kumi.
Kivuli cha mara ya kwanza kushika mkononi Dolari 1500 za kimarekani, maeneo ya mlimani city, nkaziweka chini ya godoro kwenye chumba changu cha elfu hamsini pale. Kijitonyama. kama mtu anakwambia hela haileti furaha anakudanganya, hela inapunguza stress, stress zikipungua furaha unaipata kupitia vingine. Hamna mwezi ambao nilipumua kama huu, ila kwa ajili kina sisi hatujawahi shika hela mda mrefu, kwa kweli sikumbuki iliishajeishaje hii hela, ila nilijifunza mengi sana. Hela haikai hata siku moja hata iwe nyingi kiasi gani, hata uweke benki gani kutunza, hela unaizungisha ikuletee hela zingine.
Ukisema ngoja nifanye a b na c kabla hujawekeza hela, utakuja jutia. Wekeza kwanza kisha inayobaki ndiyo tumia, I wish ningekua na huu ufahamu toka mwanzo.
Ila siku inafika hivi vitu vyote vinabaki kua vivuli tu.
Kama bado upo kwenye hali ngumu una tafuta ila Mambo hayaeleweki, nataka ujue kwamba inawezekana, inawezekana bila cheti hata kimoja, mimi nimeishia form 4 na nmeanza tafuta maisha tangu na miaka 16. Inawezekana, kuishi maisha ambayo unayaota kila siku, maisha bila stress ya hela. Inawezekana hii hali yako ya sahivi ibaki kua kivuli tu, Inawezekana. Inawezekana isiwe kesho au mwezi ujao, au hata mwaka ujao, ila weka kichwani kwamba inawezekana na tafuta njia nyingine.
Dunia ya sahivi imebadilika kinoma, kuna njia milioni moja na zaidi za kuingiza kipato. Ukijaribu moja na haijaleta mafao achana nayo jaribu nyingine, sikiliza "gut feeling" wenzetu wanaiita, jifunze mapya, tafuta connections zaidi.
Hakuna kitabu, hakuna mtu ambaye atakufundisha jinsi ya kufika unapotaka, wewe mwenyewe ndio njia utaitengeneza, angalia hizi semina za watu wanaofundisha mafanikio, anaefanikiwa ni nani kama siyo huyo anaefundisha. Hii ndo sababu pekee hutokuja niona nasema kwamba nafundisha mafanikio, hamna njia moja.
Mimi bado sijafika nnapotaka, msije mkadhani "ohh mkwanzania ameshatoka". Ila nina mda kidogo sijawaza hela ya chakula, hela ya kodi, naweza enda nnapotaka nikiamua, naweza wekeza kwenye ninachotaka. ila dah hili jiji lina vivuli vyangu vingi sana kila nikiwepo, naviona kila kona.
Kama umepitia mengi na sahivi hali imebadilika naomba tutaje vivuli unavyoviona ukipita sehemu, ili tuhamasishe watu wasife moyo, tuhamasishane tujenge jamii ya watu wanaosaidiana kufika malengo, maana kwa kweli tukiwa wachache kuna sehemu tutakwama, kipekee au kufika mwenyewe tu hatutofika mbali. Tupandishane wote, siku ije tuona watanzania wengi zaidi weusi waliotoka sifuri hadi kufika wanapotaka.
Vivuli vya zaidi ya miaka kumi ya kutafuta na kuto kubali kushindwa, vivuli vya huu mji aisee.
Vivuli vya marafiki tuliyoenda njia tofauti, vivuli vya watu uliyodhani ni marafiki, vivuli vya december na njaanuary ambapo jua linapiga hadi kero, lakini bado tunatembea na kutafuta, maana hamna njia nyingine ukiwa mtafutaji.
Hapo kati vikaja vivuli vyenye kutia moyo kidogo, kivuli cha mara ya kwanza kushika milioni moja shilingi, aisee niliona hamna kitu kinashindikana. Nikakodi chumba cha pili kuweza expand mishe, nkasema kama milioni nmeiweza kwanini nishindwe kumi.
Kivuli cha mara ya kwanza kushika mkononi Dolari 1500 za kimarekani, maeneo ya mlimani city, nkaziweka chini ya godoro kwenye chumba changu cha elfu hamsini pale. Kijitonyama. kama mtu anakwambia hela haileti furaha anakudanganya, hela inapunguza stress, stress zikipungua furaha unaipata kupitia vingine. Hamna mwezi ambao nilipumua kama huu, ila kwa ajili kina sisi hatujawahi shika hela mda mrefu, kwa kweli sikumbuki iliishajeishaje hii hela, ila nilijifunza mengi sana. Hela haikai hata siku moja hata iwe nyingi kiasi gani, hata uweke benki gani kutunza, hela unaizungisha ikuletee hela zingine.
Ukisema ngoja nifanye a b na c kabla hujawekeza hela, utakuja jutia. Wekeza kwanza kisha inayobaki ndiyo tumia, I wish ningekua na huu ufahamu toka mwanzo.
Ila siku inafika hivi vitu vyote vinabaki kua vivuli tu.
Kama bado upo kwenye hali ngumu una tafuta ila Mambo hayaeleweki, nataka ujue kwamba inawezekana, inawezekana bila cheti hata kimoja, mimi nimeishia form 4 na nmeanza tafuta maisha tangu na miaka 16. Inawezekana, kuishi maisha ambayo unayaota kila siku, maisha bila stress ya hela. Inawezekana hii hali yako ya sahivi ibaki kua kivuli tu, Inawezekana. Inawezekana isiwe kesho au mwezi ujao, au hata mwaka ujao, ila weka kichwani kwamba inawezekana na tafuta njia nyingine.
Dunia ya sahivi imebadilika kinoma, kuna njia milioni moja na zaidi za kuingiza kipato. Ukijaribu moja na haijaleta mafao achana nayo jaribu nyingine, sikiliza "gut feeling" wenzetu wanaiita, jifunze mapya, tafuta connections zaidi.
Hakuna kitabu, hakuna mtu ambaye atakufundisha jinsi ya kufika unapotaka, wewe mwenyewe ndio njia utaitengeneza, angalia hizi semina za watu wanaofundisha mafanikio, anaefanikiwa ni nani kama siyo huyo anaefundisha. Hii ndo sababu pekee hutokuja niona nasema kwamba nafundisha mafanikio, hamna njia moja.
Mimi bado sijafika nnapotaka, msije mkadhani "ohh mkwanzania ameshatoka". Ila nina mda kidogo sijawaza hela ya chakula, hela ya kodi, naweza enda nnapotaka nikiamua, naweza wekeza kwenye ninachotaka. ila dah hili jiji lina vivuli vyangu vingi sana kila nikiwepo, naviona kila kona.
Kama umepitia mengi na sahivi hali imebadilika naomba tutaje vivuli unavyoviona ukipita sehemu, ili tuhamasishe watu wasife moyo, tuhamasishane tujenge jamii ya watu wanaosaidiana kufika malengo, maana kwa kweli tukiwa wachache kuna sehemu tutakwama, kipekee au kufika mwenyewe tu hatutofika mbali. Tupandishane wote, siku ije tuona watanzania wengi zaidi weusi waliotoka sifuri hadi kufika wanapotaka.