DOKEZO Viwango vya dawa za maji DAWASCO vichunguzwe

DOKEZO Viwango vya dawa za maji DAWASCO vichunguzwe

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Mimi ni mkazi wa Kinondoni shamba, kata ya Kinondoni. Mwishoni mwa wiki iliyopita 23.11.2024 nilikunywa maji ya Dawasco ila kitu cha kushangaza yalikuwa na harufu kali sana ya dawa na pia kulikuwa na ladha ya uchungu kwa mbali.

Kwa kuwa ilikuwa weekend nilipumzika kidogo muda wa mchana. Nilipoamka nilishangaa kuona malengelenge (vipele vilivyojaa maji) kwenye kwenye ngozi mkono wa kulia na kushoto. Nikajua labda ni vipele vya joto lakini kadri nilivyoendelea kunywa yale maji, vipele vinaongezeka.

Usiku wa Jumapili jioni nikaamua kununua maji dukani ili nione kama kutakuwa na mabadiliko, leo Jumatatu nimeamka vipele vimekauka.

CENTER_0002_BURST20241125062728015.JPG
 
Nadhani ungemuona mtaalam wa afya kabla ya kuwashutumu DAWASA, huenda una magonjwa yako tu unatembea nayo
 
Back
Top Bottom