Vodacom hizi simu zenu za mikopo kwa kuzuia App za kubetia mmenikosa

Vodacom hizi simu zenu za mikopo kwa kuzuia App za kubetia mmenikosa

mr pipa

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2021
Posts
3,074
Reaction score
6,472
Tangia mwaka jana mmekuwa mkituma meseji zikinialika kutembelea duka la Vodashop lililo jirani nami ili nijipatie simu janja. Baada ya mwaka mzima wa meseji hizo kuwa kero, niliamua leo kutembelea duka na kuchukua simu yenu ili muendelee kufaidika na biashara yenu ya unyonyaji. Simu mnayouza kwa laki mbili faida yake ni laki moja, lakini siyo tatizo kwa kuwa ni malipo kidogo kidogo, buku buku kwa siku.

Nilipoingia Vodashop, muhudumu alinionesha bidhaa zenu na nilizipenda. Aliniambia nitoe namba yangu ili waone kama nakopesheka. Nilipomtajia, aliangalia kwenye mfumo na kugundua kwamba mimi siyo mtu wa mikopo, bali ninaweza kununua simu za bei kali kwa kuwa kwa siku nafanya miamala mikubwa. Kiasi cha kwamba ningeweza kukopa Samsung Galaxy 70 na kulipa yote kwa wakati mmoja. Muhudumu alizimia kwa mshtuko, nikamwagia maji ili azinduke. Alipozinduka, nikamwambia anipe masharti ya simu zenu.

Aliponiambia kuwa app za kubeti zimefungwa kwenye simu za mikopo na hazifanyi kazi hadi deni liishe, nilimwambia ameniambia jambo baya. Nikaamua sitaki kununua simu na nikaomba meseji zenu zisitumwe tena kwangu. Kwa sababu hela yenyewe ninayopata inatokana na shughuli za huko huko mlipofunga. Sikuona sababu ya kuendelea na mazoea hayo. Muhudumu alihuzunika kwa kunikosa kama mteja. Nilipotoka nje, nikakutana na meseji nyingine kutoka Vodacom ikiniomba nirudi dukani.

NB: Vodacom, simu zenu za mikopo zinatelekezwa na wateja hawalipi kwa sababu ya huu ujinga wa kufunga app za kubeti. Mmesikia uongo kwamba mkiruhusu app za kubeti kwenye simu zenu, watu hawatalipa mikopo yao? Msifanye makosa kama haya. Miamala mingi mnayopata inatokana na biashara ya kubeti. Mmefanya makosa makubwa na mnapaswa kutegemea hasara, kwa kuwa watu watazifungia ndani hizo simu.
 
mr pipa wewe ni msanii sana, sema ule uzi wako wa mishahara ya january unakuumbua

vodacom wanakujali mteja wao, yaani hata kumiliki simu huwezi unatumia ya mkopo halafu unacheza kamari? si utakosa hata hela ya kuwalipa?
 
Hawataki kushindana na mhindi kukusanya marejesho
muhind anaepukika basi?? kwenye huu uchumi mweuz wa mama juz kat nusu nilaan michezo ya kubet ile nasema hy ndio hela ya mwisho eeg mungu ninasgd mke wangu anaumwa na sina hela nikaweka buku ten mala shwaa usiku text ya sport pesa umeshinda milion 9 so naachaje kubet hata kama tunaliwa
 
mr pipa wewe ni msanii sana, sema ule uzi wako wa mishahara ya january unakuumbua

vodacom wanakujali mteja wao, yaani hata kumiliki simu huwezi unatumia ya mkopo halafu unacheza kamari? si utakosa hata hela ya kuwalipa?
wamenikosea mtumish kuna vitu vya kuzuia ila sio betting japo tunategemea mishahara ila kuna vi2 havizuiliki kwakwer
 
Ulipofika hapaa nikajua hii chai
"Nilipotoka nje, nikakutana na meseji nyingine kutoka Vodacom ikiniomba nirudi dukani."
 
muhind anaepukika basi?? kwenye huu uchumi mweuz wa mama juz kat nusu nilaan michezo ya kubet ile nasema hy ndio hela ya mwisho eeg mungu ninasgd mke wangu anaumwa na sina hela nikaweka buku ten mala shwaa usiku text ya sport pesa umeshinda milion 9 so naachaje kubet hata kama tunaliwa
Pole sana kwa kuuguza.
 
Si wanasema simu zote za mikopo hata kama sio za mitandao ya simu haziwezi ku access betting site? Sijui km ni kweli.
 
Back
Top Bottom