Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 21,741
- 26,735
"NullYou have insufficient balance to subscribe the service. But you can dial *137*09*02 to subscribe the service via M-Pesa". Hawa nao ni wale wa " ile hela tuma kwa namba hii", nao wanastahili kukamatwa.
Vodacom imekuwa na desturi ambayo ni sawa na wale wa "ile hela tuma kwa namba hii", ujumbe huu nimeuona leo alfajiri 04:47 ukidai kama unavyosomeka, huu ni moja ya ujumbe ambazo zikidai nimejiunga na sijui nini eti kila siku nilipe shs. 2
00 vinginevyo nijitoe kwa kupiga sijui -----#! Huu ni mtego kwangu mimi kwani nikipiga kujitoa naona nitakuwa nathibitisha kuwa ni kweli nilijiunga ila sasa nimeshindwa mimi, siwezi kupiga kwani nawaona ni sawa na wale wa "ile hela tuma kwa namba hii".
TCRA, yapo malalamiko mengi yanayoihusu hasa kampuni ya mtandao wa simu wa Vodacom kuhusu kuchukua hela za wateja kwa hila, mfano, unaingiza namba za vocha ili ujiunge ghafla unapata ujumbe " salio halitoshi"! Kujiunga na kifurushi cha gharama ya vocha yako, wakiwa na maana wamekukata deni unalodaiwa wakati haujawahi kukopa, hata ukijaribu kuongeza salio jingine wanakata tena na kukutumia ujumbe wa "salio halitoshi"!
Mchezo huu ni wa miaka na miaka ukiambatana na malalamiko mengi kuhusu Vodacom lakini TCRA hamchukui hatua zozote kutulinda wateja dhidi ya utapeli huu. Baadhi yetu tumekuwa na hisia ya kudhani kuwa kampuni hii na nyinginezo zina mkono wa viongozi wa CCM ndiyo sababu hamuwakamati au hamuwachukulii hatu kutokana na malalamiko ya wateja. Uchaguzi unavyokaribia ndivyo kasi ya " umejiunga kifurushi cha kuwalipa shs. 200 kila siku" inavyoongezeka.
Ninamaliza kwa kuwataka TCRA mchukueni hatua dhidi ya uhalifu huu.
Vodacom imekuwa na desturi ambayo ni sawa na wale wa "ile hela tuma kwa namba hii", ujumbe huu nimeuona leo alfajiri 04:47 ukidai kama unavyosomeka, huu ni moja ya ujumbe ambazo zikidai nimejiunga na sijui nini eti kila siku nilipe shs. 2
00 vinginevyo nijitoe kwa kupiga sijui -----#! Huu ni mtego kwangu mimi kwani nikipiga kujitoa naona nitakuwa nathibitisha kuwa ni kweli nilijiunga ila sasa nimeshindwa mimi, siwezi kupiga kwani nawaona ni sawa na wale wa "ile hela tuma kwa namba hii".
TCRA, yapo malalamiko mengi yanayoihusu hasa kampuni ya mtandao wa simu wa Vodacom kuhusu kuchukua hela za wateja kwa hila, mfano, unaingiza namba za vocha ili ujiunge ghafla unapata ujumbe " salio halitoshi"! Kujiunga na kifurushi cha gharama ya vocha yako, wakiwa na maana wamekukata deni unalodaiwa wakati haujawahi kukopa, hata ukijaribu kuongeza salio jingine wanakata tena na kukutumia ujumbe wa "salio halitoshi"!
Mchezo huu ni wa miaka na miaka ukiambatana na malalamiko mengi kuhusu Vodacom lakini TCRA hamchukui hatua zozote kutulinda wateja dhidi ya utapeli huu. Baadhi yetu tumekuwa na hisia ya kudhani kuwa kampuni hii na nyinginezo zina mkono wa viongozi wa CCM ndiyo sababu hamuwakamati au hamuwachukulii hatu kutokana na malalamiko ya wateja. Uchaguzi unavyokaribia ndivyo kasi ya " umejiunga kifurushi cha kuwalipa shs. 200 kila siku" inavyoongezeka.
Ninamaliza kwa kuwataka TCRA mchukueni hatua dhidi ya uhalifu huu.