Vodacom ni janga jipya!

MADAWA

Senior Member
Joined
Jun 21, 2013
Posts
109
Reaction score
22
Habari wana jf voda wamepandisha bei za vifurushi vya cheka bila taarifa na sababu maalumu huu ni wizi kabisa.
 
Du vida washakuwa janga aisee.....
 
Habari wana jf voda wamepandisha bei za vifurushi vya cheka bila taarifa na sababu maalumu huu ni wizi kabisa.

...kweli wameongeza bila taarifa yoyote... Nina hisi wale jamaa wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) zile kauli zao ni tisha toto... nisawa na kelele za chura... kweli mkubwa hatishiwi nyau....
 
Mimi kwangu nimekuta wamepandisha.......na akiba yangu wamekula.......niende wapi wallah mie.....
 
Au ndo bajeti imeanza kazi!!!
Jana nimeenda na 40,000/= kulipa insurance third part nikakuta imepanda hadi 100,000/= aisee huko tunakoelekea hali itakuwa mbaya mno....
 
Nyie mnaishi wapi, bunge la bajeti limeisha juzi hapa wameweka mi kodi kibao kwenye kila kitu, kuanzia Tar moja july kila kitu kimepanda bei ilaumuni serikali yenu wadau hamjashtuka tuu!
 
nilikimbia tigo kwa ajili ya usese kama huu naona na voda nao wameshiba hela wasizolipa kodi, airtell nao majanga tu...cjui nijaribu zali zantel? Mwarabu labda hana tamaa, au sijui niende sasatel? Bt hawa mikoani hawajafika...sijui twende wapi mwe.!!
 
Yap soma tarehe mbona kila kitu kimepanda Bia 2200 soda 700 nk

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
yaani wananiuzi mno yaani vyanzo vya mapato vingi mno lakini wanaumiza watu wa chini bila hatia sijui walisomea wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…