Vodacom nitawachukia milele

Vodacom nitawachukia milele

nusuhela

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2014
Posts
5,915
Reaction score
7,210
Vodacom Tanzania kama mpo humu naomba hizi habari ziwafikie. Mimi ni mteja wenu mkubwa sana. Tena mteja kindaki ndaki. Sina line ya mtandao mwingine wa simu zaidi ya line hii moja iliyonayo. Ndugu zangu wengi wapo mitandao mingine, najitahidi kumudu gharama kuwasiliana nao ili tu nisiachana na nyie.

Sasa nasema basi. Huduma yenu ya #songesha imenifanya niwachukie sana. Haiwezekani niwalipe deni lenu lote alafu mshindwe kunipa mkopo mwingine. Hilo nimelikubali na nikaamua kuachana na huo mkopo. Leo nimetumiwa hela kwaajili ya mahitaji muhimu, mmekata tena hela yote wakati sina deni na nyie.

Hakika hapa nilipo nimekasirika hakuna mfano. Maana nimewasiliana na watoa huduma wenu, wananiambia changamoto itatatuliwa ndani ya masaa 96. Hii sio haki. Hata kama ni utaratibu mliojiwekea, lakini hii haikubaliki. Hela tunazotumiana kwenye mitandao hii ya simu ni hela za mahitaji ya haraka. Leo mnaweza sababisha mtu akafatiki kwa kuikosa hiyo hela yangu ambayo ilitakiwa ikafanye mahitaji ya muhimu.

Japa nilipo mpaka naogopa kuomba hela sehemu nyingine maana inaweza ikatumwa halafu ikakatwa nikaendelea kusubilishwa masaa 96.
 
Pole sana. Kwenye haya maisha ni muhimu uwe na option B. Option A ikikwama unatumia B, mathalan tigo nivushe.

Kampuni za simu au kazi ni sawa sawa na mke. Sio kila mke ukimwacha atamiss uwepo wako.
Aisee wamenikwamisha hawa jamaa. Hela inahitajika haraka sana na nilikoomba siwezi kuomba tena. Hata nikiomba sijui nitaipataje maana wanakata hela wakati deni lao limelipwa lote jana. Nimebaki dilema najisonya tu hapa.
 
Huduma yenu ya #songesha imenifanya niwachukie sana. Haiwezekani niwalipe deni lenu lote alafu mshindwe kunipa mkopo mwingine. Hilo nimelikubali na nikaamua kuachana na huo mkopo. Leo nimetumiwa hela kwaajili ya mahitaji muhimu, mmekata tena hela yote wakati sina deni na nyie.
Mkuu ulikaa na deni lao kwa mda gani??

Labda wanalipizia 😎 😎

Nimewaza tu kwa sauti, usijekuniwashia moto
 
Mkuu ulikaa na deni lao kwa mda gani?

Labda wanalipizia 😎 😎

Nimewaza tu kwa sauti, usijekuniwashia moto
Sijakaa na deni lao muda mrefu. Mimi ni mkopaji na ninalipa kwa wakati maana natumia sana M-PESA. Kwahiyo nikitumiwa lazima ikatwe. Deni limekaa kama siku 4 tu hivi.

Jana walipokata alafu hawakunipa mkopo mwingine, nikajiongeza nikajua labda wanafanya marekebisho kwasababu mwaka wa fedha wa serikali ulianza tar 1 july. Ikabidi nifanye mchakato nipate hela nyingine. Leo asubuhi nimetumia hela, wamekata kulipia deni ambalo jana lilipiwa
 
Sijakaa na deni lao muda mrefu. Mimi ni mkopaji na ninalipa kwa wakati maana natumia sana M-PESA. Kwahiyo nikitumiwa lazima ikatwe. Deni limekaa kama siku 4 tu hivi.

Jana walipokata alafu hawakunipa mkopo mwingine, nikajiongeza nikajua labda wanafanya marekebisho kwasababu mwaka wa fedha wa serikali ulianza tar 1 july. Ikabidi nifanye mchakato nipate hela nyingine. Leo asubuhi nimetumia hela, wamekata kulipia deni ambalo jana lilipiwa
Pole mkuu.
Hamia huku tulipo sisi 😎 😎
 
hili tatzo limetokea kwa wateja wao wengi tu hivi karibuni. Kuna jamaa baada ya kulipa deni, kila akiweka hela zinakatwa zote eti kulipia deni ambalo tayari alishalipia.

Jamaa akiwapigia, majibu ni hayo hayo asubir baada ya masaa 96. Kimsingi hio huduma ya songesha ni kukaa nayo mbali sana.
 
Voda sitakaa niwasahau kipind nilituma 390,000= zikakatwa kwangu ila nilikotuma hazikwenda. Kila nikipiga simu naambiwa tatizo lako litashughulikiwa ndan ya saa 72.

Yakopita unapewa the same story, hela nilituma November nikaja kuzipata April mwaka unaofuata baada ya kumtafuta mtu ninayemfaham makao makuu. Ile line ni kama nimeitupa siku hizi na ndio ilikua line yangu ya maana.
 
Unakuwaje na line moja tena ya Voda
Nimejifunza kutokana na makosa mkuu. Nilishawahi kuwa na line za mitandao yote, ila mwisho wa siku nikaja kuona kama ni mzigo. Ila kumbe sikua sahihi kuziacha kapuni zile line nyingine
 
Back
Top Bottom