vodacom/vodafone internrt bundle wizi mtupu

mgt software

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2010
Posts
13,778
Reaction score
7,145
kwa watu wote wanaotumia modem kupata internet, amekuwepo ujanja ujanja wa vodafone kuchelewesha kujiunga baada ya kujisajiri , au wakati mwingine message za kukubaliwa haziji kabisa au zinakuja kesho yake wakati ulishakata tamaa, niliwahi kuongea nao kila saa wanasema message pending baadaye ukianza kutumia wanakujibu kuwa una hela ya kutosha kujiunga na bando au wanasema umejisajiri mara nyingi, mimi ni mtumiaji karibu miezi tano sasa wanajifanya kunifundisha wakati najua wanachofanya kwa kuwa angalau mambo ya It nayajua kwa kiwango kikubwa

vodacom/vodafone acheeeeeeeeni wiziwa bando
 
mkuu si uachane nao kama unaona wanakuibia hao
 
If you can not solve the problem then you are the part of that problem. Kwanini usiwahame?!
 
Kupanga ni kuchagua, achana nao - biashara huria siku hizi
 
Na sisi wa Airtel huo usanii upo sana tu, na kinachokera zaidi kama line yako ina pesa na umeweka data siku ya mb 20, basi zikiisha hizo mb 20 hawakutumii msg kwamba zimekwisha na wanaanza kukukata kwa mtindo wa pay as you go. nchi hii ni wizi mtupu kila sekta.
 
Hawa jamaa wa Vodacom ni wasanii kwelikweli. Nimenunua data 250MB imetumika mwezi mzima, ilipoisha nikanunua tena 250MB ikatumika siku tatu, yaani hawaeleweki kabisa. Cha kufanya kamata modem zote mbili uwe una alternate. Ila siku hizi wameimprove katika kasi ya internet kupitia HSPDA yenye 3.5G, sasa waweke bei hadharani kama ilivyo kwa airtme ili usanii huu wanaotufanyia katika internet ukome. Wizi mtupu vodacom
 
Hawa jamaa kwa kweli ni wezi sana..
 


kaka mimi pia ni mtumiaji wa Vodacom Internet Bundle ya mwezi mzima na nimekuwa na tatizo hilo hilo kila ninapomaliza package yangu na kujiunga tena, niliwafuata ofisini ili nijue sababu nikagundua kwamba line za Vodacom za zamani zina matatizo katika Database yao ya Internet na hivyo request huchelewa kuwa processed. nimenunua line nyingine wiki iliyopita na tatizo limeisha...Jaribu kufanya hivyo naamini itakusaidia na wewe...otherwise, with 3.5G, vodacom Unlimited Int' Service is the best of all :A S 101:
 
Mimi natumia Zantel, huku nako ni ujanjaujanja tu unatumika. Kuna hiyo kitu wanaita Highlife package, masharti yake yamefichika fichika yaani wizi mtupu.
Nilikuwa nawashangaa watu wanaochakachua sasa nimeanza elewa kumbe ni hizi kero.
Wanaotumia tigo wameniambia wanafurahia, naomba mnijulishe kama naweza tumia modem ile ile ya zantel kuunganishwa na tigo, aina yake ni ZTE.
 
Mkuu mimi nilishaachana nao siku nyingi nilishagundua hayo magumashi, nimenunua EVDO Modem ya TTCL wameniunganisha na Banjuka, aisee acha kabisa, speed ya ukweli, no outage yani ni fasta na raha. Changamoto yao ni coverage tu lakini TTCL ni best of all na sio wevi kama voda, tigo, zain na zantel
 
Mkuu hapo penye red, nakushauri fuatilia maana ya penetration strategy na nini hufanyika ili ufanikishe hiyo strategy as far as marketing & sales is concerned
 
Wizi Jazz Band
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…