Vodacom wazindua simu za wasioona,wasiosikia

kilimasera

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2009
Posts
3,068
Reaction score
277
KAMPUNI ya simu ya mkononi ya Vodacom Tanzania, imezindua simu maalum kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa macho na matatizo ya kusikia zitakazoweza kuwasaidia kutumia simu hizo.
Akizungumza na wwanahabri wakati wa uzinduzi ,Meneja Mawasiliano wa kampuni hiyo, Nector Foya, alisema simu hizo ni tofauti na nyingine kwa kuwa zitawawezesha wateja kundi hilo kutmia simu hizo kama wengine na kupata huduma ambazo hazipo katika simu za kawaida.

Simu hizo zimewekwa maandishi makubwa katika Keypad, sauti kubwa katika spika na king'ora maalum nyuma ya simu kitakachowawezesha makundi hayo kukibonyeza wakati wa dharura.

Alisema Vodacom imemua hivyo kutokana na kugundua kuna watanzania wengi wanapata shida katika kutumia simu za kawaida ka kuwa na maandishi madogo, sauti ndogo na wengi huhitaji malekezo kutoka kwa watu wengine pindi anapohitaji kutumia simu.
 
safi sana kwa kuwakukumbuka walemavu i hope zitakuwa msaada sana kwao ila na wasifu sana walemavu niliobahatika kuonana nao wanatumia cm kwa kweli nilistahajabu kwa jinsi alivyokuwa na kipaji cha ajabu alikuwa na cm ya philips savy za zamani sana akanipa akawa ananielekeza bonyeza hapo kati, eehe imesema menu eeh,bonyeza mchale wa kulia imeandika call hivyo me hoi mpaka cm anapiga na akipokea anajua anaongea na nani ukisema tu aloo yy anakutaja jina nilibaki mdomo wazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…