Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 25,252
- 36,513
Tumemsikia kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo bwana Zitto pale Mbagala Zakhem akitueleza Watanzania namna mambo ya ajabu yanayoendelea Bungeni.
Amesema kwa ufasaha kuwa kifungu namba 20 cha bajeti ambacho kina fedha za Takukufu, Usalama wa Taifa na matumizi binafsi ya Rais kimewekewa zuio na sheria za Bunge kutojadiliwa. Hivyo kinapitishwa bila kuhojiwa na hesabu zake zinapokelewa bila kujadiliwa.
Nimejiuliza, kifungu hiki namba 20 kina source gani ya fedha nje ya kodi zetu? Rais anapotueleza kuwa kodi zetu ni muhimu kuzihoji matumizi yake lakini hatuelezi kwamba kuna fedha haturuhusiwi kuhoji matumizi yake kwa sababu tunaingilia usalama wa nchi?
Kiukweli siyo jambo la busara hata kidogo kutaka kuwafahamu maafisa vipenyo kwa sababu za usalama wa nchi, lakini hatuwezi kuona ni busara kutokujua uhalali wa matumizi ya fedha zetu za kodi kwa taasisi hizo hususan TISS na TAKUKURU. Hizi mbinu za kujengeana hofu zinatoa nafasi kwa wasio waaminifu kutapanya rasilimali za taifa bila kuwajibishwa. Kama kuna maafisa vipenyo ambao wanakiuka viapo vyao na kuwajibishwa, je kuna utakatifu gani uliotukuka kwenye eneo la matumizi ya fedha? Tusisahau ike kashfa ya DEEP GREEN ambapo mpaka leo hakuna aliyewajibishwa kwa ufisadi ule. Ilisemwa bungeni kwamba fedha zilizopelekwa kwenye akaunti za Deep Green zilitumika kwa.masuala ya usalama wa Taifa...... kesi ikazimishwa hapo
Kifungu namba 20 pia kinahusika na matumizi binafsi ya Rais. Tunampenda na kumuenzi rais wetu. Pia tunamuomba aangalie hili jambo kwa kina. Yeye ni taswira ya Taifa na pia raia namba moja. Tunapenda kumuona akiishi kama mfano katika eneo la.matumizi. hatuwezi kumuona anatumia fedha vibaya pale anapokuwa anatoa fedha kwa wananchi wenye shida mbali mbali.
Pia tunajua kuwa kazi anayoifanya ni ngumu, hivyo kifungu hiki kimhusu yeye zaidi na siyo taasisi nyeti z serikali. Nashauri kifungu hiki ambacho ndicho msingi wa madaraka makubwa ya kimungu kwa rais kiwe na subsections ambapo kila section isimame kwa clarity yake yaani tusihoji matumizi binafsi ya Rais lakini mapato na matumizi ya TISS na TAKUKURU yawe bayana kwa ajili ya kuimarisha utawala bora na uwazi kwenye fedha za umma.
Ikiwezekana fungu la masuala ya ulinzi na usalama yatenganishwe na matumizi binafsi ya Rais kwa sababu tunajuaje endapo fedha hizo zilitumika ama zitatumika kukandamiza haki za binadamu na kuathiri usalama wa raia kama taifa ili kustawisha usalama wa taasisi kwa kivuli cha usalama wa taifa.
KATIBA mpya ituletee taasisi imara na siyo kuimarisha sheria zinazosimamia ofisi yenye mkuu mmoja ambaye anaweza akaja shetani kukalia kiti na nchi yote kugeuka jehanamu ya moto ambayo funza wake hawafi.
Enewei
Tujadili kwa kuzingatia umuhimu wa usalama wa nchi. Lakini tuangalie umuhimu wa kuondoa makandokando yanayopelekea taasisi zetu za muhimu kunyooshewa vidole.
Mshana Jr Retired Ushimen raraa reree Mchambuzi MALCOM LUMUMBA zitto junior Lucas mwashambwa Voice of Hope 2022 figganigga Nyani Ngabu Ex Spy EagleEyed
Amesema kwa ufasaha kuwa kifungu namba 20 cha bajeti ambacho kina fedha za Takukufu, Usalama wa Taifa na matumizi binafsi ya Rais kimewekewa zuio na sheria za Bunge kutojadiliwa. Hivyo kinapitishwa bila kuhojiwa na hesabu zake zinapokelewa bila kujadiliwa.
Nimejiuliza, kifungu hiki namba 20 kina source gani ya fedha nje ya kodi zetu? Rais anapotueleza kuwa kodi zetu ni muhimu kuzihoji matumizi yake lakini hatuelezi kwamba kuna fedha haturuhusiwi kuhoji matumizi yake kwa sababu tunaingilia usalama wa nchi?
Kiukweli siyo jambo la busara hata kidogo kutaka kuwafahamu maafisa vipenyo kwa sababu za usalama wa nchi, lakini hatuwezi kuona ni busara kutokujua uhalali wa matumizi ya fedha zetu za kodi kwa taasisi hizo hususan TISS na TAKUKURU. Hizi mbinu za kujengeana hofu zinatoa nafasi kwa wasio waaminifu kutapanya rasilimali za taifa bila kuwajibishwa. Kama kuna maafisa vipenyo ambao wanakiuka viapo vyao na kuwajibishwa, je kuna utakatifu gani uliotukuka kwenye eneo la matumizi ya fedha? Tusisahau ike kashfa ya DEEP GREEN ambapo mpaka leo hakuna aliyewajibishwa kwa ufisadi ule. Ilisemwa bungeni kwamba fedha zilizopelekwa kwenye akaunti za Deep Green zilitumika kwa.masuala ya usalama wa Taifa...... kesi ikazimishwa hapo
Kifungu namba 20 pia kinahusika na matumizi binafsi ya Rais. Tunampenda na kumuenzi rais wetu. Pia tunamuomba aangalie hili jambo kwa kina. Yeye ni taswira ya Taifa na pia raia namba moja. Tunapenda kumuona akiishi kama mfano katika eneo la.matumizi. hatuwezi kumuona anatumia fedha vibaya pale anapokuwa anatoa fedha kwa wananchi wenye shida mbali mbali.
Pia tunajua kuwa kazi anayoifanya ni ngumu, hivyo kifungu hiki kimhusu yeye zaidi na siyo taasisi nyeti z serikali. Nashauri kifungu hiki ambacho ndicho msingi wa madaraka makubwa ya kimungu kwa rais kiwe na subsections ambapo kila section isimame kwa clarity yake yaani tusihoji matumizi binafsi ya Rais lakini mapato na matumizi ya TISS na TAKUKURU yawe bayana kwa ajili ya kuimarisha utawala bora na uwazi kwenye fedha za umma.
Ikiwezekana fungu la masuala ya ulinzi na usalama yatenganishwe na matumizi binafsi ya Rais kwa sababu tunajuaje endapo fedha hizo zilitumika ama zitatumika kukandamiza haki za binadamu na kuathiri usalama wa raia kama taifa ili kustawisha usalama wa taasisi kwa kivuli cha usalama wa taifa.
KATIBA mpya ituletee taasisi imara na siyo kuimarisha sheria zinazosimamia ofisi yenye mkuu mmoja ambaye anaweza akaja shetani kukalia kiti na nchi yote kugeuka jehanamu ya moto ambayo funza wake hawafi.
Enewei
Tujadili kwa kuzingatia umuhimu wa usalama wa nchi. Lakini tuangalie umuhimu wa kuondoa makandokando yanayopelekea taasisi zetu za muhimu kunyooshewa vidole.
Mshana Jr Retired Ushimen raraa reree Mchambuzi MALCOM LUMUMBA zitto junior Lucas mwashambwa Voice of Hope 2022 figganigga Nyani Ngabu Ex Spy EagleEyed