VPL: Mwadui yaendelea kushika mkia msimamo wa ligi kuu

VPL: Mwadui yaendelea kushika mkia msimamo wa ligi kuu

Shadida Salum

Journalist at JamiiForums
Joined
Sep 11, 2020
Posts
69
Reaction score
105
20210216_182748.jpg

Baada ya kuondoka na alama moja katika mchezo dhidi ya Kagera sugar juma lililopita, Gwambina hii leo ameambulia patupu baada ya kuruhusu kichapo cha bao 1-0 akiwa katika Dimba la nyumbani dhidi ya Ruvu Shooting.

Goli la Ruvu shooting lilifungwa na F Ikobela 47'.

Na katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam KMC wamefanikiwa kuweka kibindoni alama tatu muhimu baada ya kumchapa Mwadui goli 2-1.

Matokeo haya yanajirudia kwa Mwadui baada ya kufungwa goli 2-1 na Biashara katika Dimba la Mwadui complex Juma lililopita.

Magoli ya KMC yamefungwa na E Mvuyekure 13' na C Ilanfya, huku goli la Mwadui likifungwa na D Richard 70'.
 
Mwadui FC wamekosa kushuka daraja misimu miwili mfufulizo Safari hii hiki kikombe hawatakieupuka naamini wanashuka daraja!
 
Back
Top Bottom