Vunja mifupa ngali meno bado iko...

Huwa naburudika sana na huu wimbo. Asante sana mwanakijiji
 
SIKILIZA HAPA

Fikiria uko kilabuni tena kile cha mataputapu au cha karibu na duka la fulani..

Dah....ebana huu wimbo umenikumbusha enzi hizo pale Mwenge karibu na kambi ya jeshi ya ujenzi....kulikuwaga na mgahawa/baa/klabu moja hivi ilikuwa inaitwa Tarakea....walikuwaga wanapika mtori wa nguvu....halafu walikuwaga wanauza na chibuku (hivi hii nayo inahesabika kama pombe ya kienyeji? lol)....yaani nikikumbuka enzi hizo hadi machozi yananilengalenga aiseee

Nimekunywa sana chibuku (tulikuwa tunanywea mavikombe flani hivi makubwa) pale huku wimbo huu ukidunda kwenye maspika...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…