Muuza Kangala
JF-Expert Member
- Jul 21, 2021
- 1,242
- 4,813
Mbunge wa jimbo la Ulanga Salim Alaudin Hasham ametembelelea katika kata ya Mwaya kujionea uharibifu uliojitokeza wa daraja kuvunjika na kusababisha kata nne za Mwaya, Ilonga, Mbuga na Ketaketa kukosa mawasiliano
Mbunge Salimu amesema kwa sasa ameishatoa taarifa ya changamoto hiyo kwa mamlaka husika na hatua za haraka zitachukuliwa huku akiwapongeza wananchi kwa kujitolea michango ya fedha kiasi cha shilingi 1,200,000 kwa ajili ya kivuko cha muda naye tayari ametoa kiasi cha fedha shilingi 1,000,000 huku Mwenyekiti wa Halmashauri akichangia kiasi cha shilingi 300,000 na jumla kupatikana kiasi cha shilingi 2,500,000
Pia Mbunge Salimu amewataka wananchi kushirikiana na wataalamu katika ujenzi wa kivuko hicho cha muda kipindi ambacho anaendelea kupambana kupata daraja imara ili kuweza kurejesha huduma za kijamii kama awali
Mbunge Salimu amesema kwa sasa ameishatoa taarifa ya changamoto hiyo kwa mamlaka husika na hatua za haraka zitachukuliwa huku akiwapongeza wananchi kwa kujitolea michango ya fedha kiasi cha shilingi 1,200,000 kwa ajili ya kivuko cha muda naye tayari ametoa kiasi cha fedha shilingi 1,000,000 huku Mwenyekiti wa Halmashauri akichangia kiasi cha shilingi 300,000 na jumla kupatikana kiasi cha shilingi 2,500,000
Pia Mbunge Salimu amewataka wananchi kushirikiana na wataalamu katika ujenzi wa kivuko hicho cha muda kipindi ambacho anaendelea kupambana kupata daraja imara ili kuweza kurejesha huduma za kijamii kama awali