Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,872
- 34,363
VYAKULA VILIVYOUNGUWA (CHIPS) VINASABABISHA UGONJWA WA
KENSA TUJIHADHARI SANA KULA HIVYO VYAKULA.
Wanasayansi wanasema kuwa wanawake ambao hula chips au 'crips' kila siku wanaweza kuongeza mara mbili hatari ya kensa ya kizazi na ya ovari.
Hatari hiyo inatokana na mada iitwayo acrylamide, ambayo hupatikana wakati wa kukaanga, kuoka au kuchoma vyakula mbalimbali. Wataalamu
wa Kidachi wamewafanyia uchunguzi watu 120,000 juu ya tabia yao ya ulaji na kugundua kuwa wanawake ambao wanakula vyakula vyenye
acrylamide, wanaonekana kukabiliwa na hatari zaidi ya kupatwa na aina hizo za saratani. Vyakula ambavyo vinapata rangi mbalimbali au kuungua
wakati wa kupikwa vinaonekana kuwa na uwezekano mkubwa zaidi wa kuwa na acrylamide. Wataalamu wa vyakula wanasema kuwa, ni wazi kuwa
haiwezekani kuondoa aina hizo za vyakula moja kwa moja katika lishe yetu. Uchunguzi kuhusiana na masuala hayo umeonyesha kuwa, wale ambao wanakula mikrogram 40 za acrylamide kwa siku ambayo ni sawa na nusu
ya pakiti ya biskuti, sahani ya chipsi ya paketi moja ya crisp, basi wanakabiliwa na hatari ya kupatwa na kensa mara mbili zaidi ikilinganishwa
na wale wanaokula acrylamide kwa kiasi kidogo zaidi ya hicho. Hata hivyo wataalamu wa uchunguzi huo wanawatoa shaka watu kwa kusema kuwa, matokeo ya uchunguzi huo yanapaswa kuthibitishwa zaidi na uchunguzi mwingine.