Pre GE2025 Vyama vyote ambavyo ni wapinzani wa CCM, hawawatendei haki wapenzi wao, Daftari la kudumu la Wapiga Kura

Pre GE2025 Vyama vyote ambavyo ni wapinzani wa CCM, hawawatendei haki wapenzi wao, Daftari la kudumu la Wapiga Kura

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Ghiti Milimo

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2011
Posts
4,748
Reaction score
7,061
Wakuu, heshima kwenu!

Moja kwa moja kwenye hoja yangu.

Hivi karibuni 'Tume huru ya Taifa ya uchaguzi', ilitangaza kuanza kuandikisha/kuboresha/kurekebisha daftari la kudumu la wapiga kura, kwa wakazi wa Mkoa wa Mwanza na Shinyanga, kuanzia tarehe 21 August, 2024 mpaka tarehe 27 August, 2024. Vyama vyote vyenye usajili, vinatakiwa kuwa na wawakilishi/mawakala kwa kila kituo, kwa ajili ya kushuhudia hao wanaoandikishwa.

Cha kushangaza, kuanzia hiyo tarehe 21 August, 2024,mimi binafsi, nimezungukia vituo vinne vya kuandikishia hapa Shinyanga mjini, ni kituo kimoja tu, ndicho nimewakuta mawakala wawili, ikiwa ni wa CCM na wa CHADEMA.

Hivyo vingine vitatu, vina Wakala mmoja mmoja, ambao ni wa CCM peke yao. Na nikanong'onezwa kuwa, CCM inao Mawakala wengine wapo stand by, ikitokea dharula kwa Wakala wa kituo chochote, anakwenda kuchukua nafasi. Pia, nimeshuhudia, Makada wao, wakiwahamasisha wapenzi wao, kwenda kujiandikisha.

Soma Pia: Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, wapiga kura wapya 190,131 wanatarajiwa kuandikishwa Mwanza

Sasa, unajiuliza, hivi, tofauti na CCM, hao wengine, wapo tayari kwa mapambano? Pamoja na kuwa ni vigumu kuzuia kila hujuma, lakini kwa style hii, watapona kweli? Hivi yale aliyo "ropoka" Nape Nnauye, wanafikiri ni utani? Hivi, baada ya Uchaguzi, watakuwa na uhalali wa kulalamikia WAPIGA KURA HEWA, au VITUO HEWA?

Vyama vyote ambavyo ni wapinzani wa CCM, hawawatendei haki wapenzi wao! Wanawachosha, na kuwakatisha tamaa kuwaunga mkono!
 
Wakuu, heshima kwenu!
Moja kwa moja kwenye hoja yangu.
Hivi karibuni 'Tume huru ya Taifa ya uchaguzi', ilitangaza kuanza kuandikisha/kuboresha/kurekebisha daftari la kudumu la wapiga kura, kwa wakazi wa Mkoa wa Mwanza na Shinyanga, kuanzia tarehe 21/08/2024 mpaka tarehe 27/08/2024. Vyama vyote vyenye usajiri, vinatakiwa kuwa na wawakirishi/mawakala kwa kila kituo, kwa ajili ya kushuhudia hao wanaoandikishwa.
Cha kushangaza, kuanzia hiyo tarehe 21/8/2024,mimi binafsi, nimezungukia vituo vinne vya kuandikishia hapa Shinyanga mjini, ni kituo kimoja tu, ndicho nimewakuta mawakala wawili, ikiwa ni wa CCM na wa CHADEMA. Hivyo vingine vitatu, vina Wakala mmoja mmoja, ambao ni wa CCM peke yao.
Na nikanong'onezwa kuwa, CCM inao Mawakala wengine wapo stand by, ikitokea dharula kwa Wakala wa kituo chochote, anakwenda kuchukua nafasi. Pia, nimeshuhudia, makada wao, wakiwahamasisha wapenzi wao, kwenda kujiandikisha.
Sasa, unajiuliza, hivi, tofauti na CCM, hao wengine, wapo tayari kwa mapambano? Pamoja na kuwa ni vigumu kuzuia kila hujuma, lakini kwa style hii, watapona kweli? Hivi yale aliyo "ropoka" Nape Nnauye, wanafikiri ni utani? Hivi, baada ya uchaguzi, watakuwa na uhalali wa kulalamikia WAPIGA KURA HEWA, au VITUO HEWA?
Vyama vyote ambavyo ni wapinzani wa CCM, hawawatendei haki wapenzi wao! Wanawachosha, na kuwakatisha tamaa kuwaunga mkono!

Kuna aliyewahi viita Saccos:

Kusuasua kwa harakati za ukombozi nchini ni matokeo ya uongozi dhaifu

Kwamba kuna wenye kuamini kwenye kupewa si kupigania.

Safari ingali ndefu!

Cc: imhotep
 
Wakuu, heshima kwenu!
Moja kwa moja kwenye hoja yangu.
Hivi karibuni 'Tume huru ya Taifa ya uchaguzi', ilitangaza kuanza kuandikisha/kuboresha/kurekebisha daftari la kudumu la wapiga kura, kwa wakazi wa Mkoa wa Mwanza na Shinyanga, kuanzia tarehe 21/08/2024 mpaka tarehe 27/08/2024. Vyama vyote vyenye usajiri, vinatakiwa kuwa na wawakirishi/mawakala kwa kila kituo, kwa ajili ya kushuhudia hao wanaoandikishwa.
Cha kushangaza, kuanzia hiyo tarehe 21/8/2024,mimi binafsi, nimezungukia vituo vinne vya kuandikishia hapa Shinyanga mjini, ni kituo kimoja tu, ndicho nimewakuta mawakala wawili, ikiwa ni wa CCM na wa CHADEMA. Hivyo vingine vitatu, vina Wakala mmoja mmoja, ambao ni wa CCM peke yao.
Na nikanong'onezwa kuwa, CCM inao Mawakala wengine wapo stand by, ikitokea dharula kwa Wakala wa kituo chochote, anakwenda kuchukua nafasi. Pia, nimeshuhudia, makada wao, wakiwahamasisha wapenzi wao, kwenda kujiandikisha.
Sasa, unajiuliza, hivi, tofauti na CCM, hao wengine, wapo tayari kwa mapambano? Pamoja na kuwa ni vigumu kuzuia kila hujuma, lakini kwa style hii, watapona kweli? Hivi yale aliyo "ropoka" Nape Nnauye, wanafikiri ni utani? Hivi, baada ya uchaguzi, watakuwa na uhalali wa kulalamikia WAPIGA KURA HEWA, au VITUO HEWA?
Vyama vyote ambavyo ni wapinzani wa CCM, hawawatendei haki wapenzi wao! Wanawachosha, na kuwakatisha tamaa kuwaunga mkono!
Naomba nikusaidie kupunguza frustration zako. CCM haitatolewa na box la kura. Kuna siku wasiotegemea wananchi watawatoa kupitia maandamano ya vurugu na umwagaji damu. Huu ni mtazamo wangu.
 
Taifa hili halina Tume ya uchaguzi wala uchaguzi wa uhuru na haki.Ni mpumbavu tu,ndo atashiriki chaguzi za kipumbavu.
 
Naomba nikusaidie kupunguza frustration zako. CCM haitatolewa na box la kura. Kuna siku wasiotegemea wananchi watawatoa kupitia maandamano ya vurugu na umwagaji damu. Huu ni mtazamo wangu.
vurugu sio kwa nchi hii
 
Back
Top Bottom