Vyombo vya Habari ni kitu Muhimu na kisichoepukika ili kuwa na Uchaguzi huru na wa Haki

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Zipo seti kuu mbili za dhima za Vyombo vya Habari nyakati za uchaguzi, ya kwanza inatokana na msimamo wa Kitaaluma ikiunganishwa na Wajibu wao kwa jamii, ya pili ni wajibu wa Kisheria wa Vyombo vya Habari.

Andiko la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kuhusu Vyombo vya Habari na Uchaguzi Mkuu 2020 linaeleza Vyombo vya Habari hutekeleza wajibu wake kwa kuarifu, kuelimisha, na hatimaye kuwajengea uwezo Wananchi kwa kuwapatia taarifa sahihi, zinazotoka kwa wakati, zilizowekwa kwenye muktadha, zilizofanyanyiwa utafiti na zinazohusiana na mchakato mzima wa Uchaguzi.

Hii inajumuisha kuwaleta pamoja raia ili kuchukua hatua na kushiriki kwenye chaguzi. Hivyo, Vyombo vya Habari ni kitu muhimu na kisichoepukika ili kuwa na Uchaguzi huru na wa Haki.
 

Attachments

Mkuu Roving Journalist , asante sana kwa hii kitu naifanyia kazi.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…