Nimekuwa nikijiuliza muda mrefu sana kwa nini vyuo vikuu vya Tanzania havina matawi yake ktk nchi za Africa Mashariki ingali huku Serikali ya Tanzania ikiwahimiza Watanzania kuchangamkia fursa za ajira wakati hata vyuo vikuu vyake vinashindwa kuwa na matawi katika nchi za Afrika Mashariki.
Wenzetu Kenya na Uganda wamejitahidi kuchangamkia fursa ya kielimu kwa kufungua matawi ya vyuo vyao vikuu.
Mfano Kampala University wana tawi Dar es Salaam na Jomo Kenyatta University wana tawi lao Arusha.
Na hatimaye Open University of Tanzania (OUT)hatimaye wamevunja ukimya nadhani wana tawi Nairobi maana nimeona tangazo lao kupitia Citizen Tv ya Kenya kwa kushirikiana na Institute of Human Resource Management cha Kenya.
Vyuo vingine vinangoja nini au ndo ukiritimba?
Vyuo vikuu vingine vya Tanzania muige mfano huu.
Wenzetu Kenya na Uganda wamejitahidi kuchangamkia fursa ya kielimu kwa kufungua matawi ya vyuo vyao vikuu.
Mfano Kampala University wana tawi Dar es Salaam na Jomo Kenyatta University wana tawi lao Arusha.
Na hatimaye Open University of Tanzania (OUT)hatimaye wamevunja ukimya nadhani wana tawi Nairobi maana nimeona tangazo lao kupitia Citizen Tv ya Kenya kwa kushirikiana na Institute of Human Resource Management cha Kenya.
Vyuo vingine vinangoja nini au ndo ukiritimba?
Vyuo vikuu vingine vya Tanzania muige mfano huu.