SI KWELI Vyuo vya UDSM, UDOM, IFM na SUA vinaongoza kwa maambukizi ya VVU nchini Tanzania

SI KWELI Vyuo vya UDSM, UDOM, IFM na SUA vinaongoza kwa maambukizi ya VVU nchini Tanzania

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
IMG_8963.jpeg
 
Tunachokijua
Novemba 3, 2023, Ukurasa unaopatikana kwenye mtandao wa X unaofahamika kwa jina la Tanzania Abroad TV ulichapisha habari inayoonesha idadi ya visa vya maambukizi ya UKIMWI kwenye baadhi ya vyuo nchini.

Chapisho hilo lilisema:

“Tumia kinga uwa leo vyuo hivi….UDSM Ina wanafunzi wa UKIMWI 16,000. UDOM Ina wanafunzi wa UKIMWI 8,682. IFM Ina wanafunzi wa UKIMWI 4,526. SOKOINE Ina wanafunzi wa UKIMWI 3,521. Mzumbe wenye UKIMWI ni 3,236”

Hadi kufikia Novemba 6, 2023, chapisho hili lilikuwa limesomwa na zaidi ya watu 163,00, watu 1329 walilipenda huku wengine 126 wakishirikisha wengine. Aidha, watu 76 walihifadhi chapisho hili (Bookmark) kwa ajili ya kumbukumbu na matumizi ya baadae.

Ukweli wa takwimu hizi upoje?
Baada ya kusambaa kwa taarifa hizi, JamiiCheck ilifanya jitihada kadhaa, ikiwemo kufuatilia hotuba za Waziri wa Afya Ummy Mwalimu na Naibu wake Dkt. Mollel pamoja na kurejea nyaraka za taarifa rasmi za kiserikali zenye kufafanua na kutoa taswira ya maambukizi ya VVU nchini.

Katika ufuatiliaji huu, JamiiCheck haikupata chanzo chochote cha kuaminika kilichotoa taarifa hizi. Aidha, takwimu tajwa hazipatikani sehemu zingine isipokuwa kwenye ukurasa wa Tanzania Abroad TV jambo linalotia shaka ukweli wake.

Kanusho la Mamlaka
Novemba 3, 2023, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu alikanusha taarifa hii kupitia mtandao wa X.

Pia, Novemba 4, 2023, Ukurasa rasmi wa Wizara ya Afya kwenye mtandao wa X ulikanusha taarifa hii kwa kuiita kuwa ni "Uzushi" na kuwataka wananchi waipuuze.

F-D5WkxWIAAnTFS

Kanusho la Wizara ya Afya kwenye mtandao wa X
Kwa mujibu wa Utafiti wa mwaka 2022/23 uliofanywa na Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS), Tume ya Kudhibiti UKIMWI Zanzibar (Zanzibar AIDS Commission- ZAC), Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) pamoja na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Zanzibar, Tanzania imepata matokeo chanya katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI na kwamba idadi ya maambukizi mapya inaendelea kupungua ikilinganishwa na matokeo ya utafiti wa mwaka 2026/17.

Kushiriki tendo la ndoa, kupokea damu na mazao yake, uchangiaji wa vifaa vyenye ncha kali pamoja na maambukizi ya mama kwa mtoto wakati wa ujauzito na (au) wakati wa kujifungua ni baadhi ya njia zilizothibitishwa kuwa na uwezekano usiotia shaka katika kusababisha maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) ambapo ikiwa tiba sahihi haitatolewa, mtu huyu hupata Upungufu wa Kinga Mwilini (UKIMWI) ambayo ni hatua kubwa zaidi ya maambukizi.

Tangu kugunduliwa kwake zaidi ya miaka 40 iliyopita, zaidi ya watu milioni 85.6 wameambukizwa ugonjwa huu huku takriban watu milioni 40.4 wakipoteza maisha. Hii ni kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO).

Aidha, hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2022, takriban watu milioni 39 walikuwa wanaishi na maambukizi ya ugonjwa huu duniani.
Hizi takwimu wamepataje?? Hii inatisha..
 
Acha wakavune maradhi badala ya maarifa kwa kuhendekeza ngono
 
Hii social media iliyotumika kutoa takwimu za uongo iwajibishwe kisheria
 
Sasa kama ni uzushi, taarifa rasmi yenye takwimu ni ipi? maana ili tubalance story tusikie pande zote mbili tujue, vinginevyo raia wataendelea kuamini hiyo "Tweet"

Kukanusha bila takwimu za hayo maambukizi vyuoni mi naona ni uongo
 
sasa kama pale riverside asilimia ya wauza nyapu wote wanatoka mabibo hostel unategemea nini, na IFM ni kwakuwa serikali imehama tu yaanin watoto wale wanauza hadi wanaogopesha Ohio yoooote viwanja vya Golf mpaka Agakhan wanajaa usiku kama siafu yaani hili janga ni kubwa sana wandugu.
 
Back
Top Bottom