Waafrika tutajitambua lini na kuachana na ukoloni wa kidini na kimila hata kiuchumi?

Waafrika tutajitambua lini na kuachana na ukoloni wa kidini na kimila hata kiuchumi?

Father of All

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
7,672
Reaction score
9,039
Akiitwa Mjapan utasikia Mashayoshi Ohira.
Akiitwa mchina utasikia Nie Hon Hun.
Akiitwa mzungu utasikia John, Michael nk.
Akiitwa mmanga utasikia Mohamed bin Suleiman.
Akiitwa gacholi utasikia Kanji Mahendra.
Akiitwa mswahili utasikia John Mohamed Michael nk.
Je waswahili tutajitambua na kujikubali lini na kuacha kutumikia ujinga wa watu?
Israel ikipigana na Palestina tunagawanyika kwenye makundi ya kijiinga ya wakristo na waislam.
Tukipigana sisi kwa sisi wenzetu wala hawajali wala kuona.
Tunaimba na kucheza muziki wa wenzetu na kuogopa na kuchukia wetu.
Tunaapa kwa vitabu vyao wakati hawaapi kwa vyetu.
kila chetu ni haramu isipokuwa madini, vyakula na utajiri na nguvu yetu.
Miji yetu tunakwenda kuhiji eti ni mitakatifu kana kwamba yetu ni michafu. Tunakwenda kule kusujudia makaburi na misalaba yao.
Tutaamka lini na kuasi uzwazwa huu?
 
Back
Top Bottom