Waafrika wamelaaniwa: Hichilema utafanya yaleyale ya Lungu ya kuonea Wapinzani

Waafrika wamelaaniwa: Hichilema utafanya yaleyale ya Lungu ya kuonea Wapinzani

Retired

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2016
Posts
44,629
Reaction score
83,056
Ni wazi mgombea wa upinzani nchini Zambia atatangazwa mshindi.

My concern is: Historia inatukumbusha kuwa Hichilema aliwekwa ndani na Lungu kwa kumpa kesi ya kumbambikia ya Uhaini. Mahakama ikamweka huru.

Kwa akili za Waafrika tulivyolaaniwa, huyu mteule Hichilema atafanya hayo hayo kwa Wapinzani wake Mara akiapishwa.

It is a matter of some few days to come we will witness atrocities commanded by him against opposition
 
Huwezi jua mkuu labda yeye hana nia ovu kama hizo lakini pia usimfananishe na huyu wa kwetu hapa, yeye karithi hajapigania icho kiti na pia huyu wetu kafungwa lwenye mfumo wa chama chake kama cha aliepita kwahiyo nae anapita mulemule na kuongeza yake.
 
Wa Afrika ndivyo tulivyo! Huwa hatupiganii kuongoza wananchi bali hupigania matumbo yetu na kuwatawala wananchi badala ya kuwaongoza.

Ukiwa mtawala utataka kukaa kwenye utawala milele hivyo utawaona wapinzani wako ni maadui na utawashughulikia.

Issue ya Mbowe ni suala tofauti siyo kama huko kwingine
 
Hizo ni hisia zako tu, pengine asimfanyie kama unavofikiria na badala yake akaomba ushirikiano kwake, sababu wazambia wameiva kidemokrasia sawa na wazungu.
 
Mimi nadhani kuikomesha tabia hii ni kumtenda aliyekutenda au aliyewatenda wengine alipokuwa madarakani na sio kuendeleza tabia kwa wapya.

Mfano, Hichilema ahakikishe Lungu anayapata machungu kulipa aliuofanya.

Au hapa kwetu mfano CCM inaondolewa madarakani, basi wale wote walio tesa watu kwa makusudi wakitumia madaraka na uchama wao waipate fresh bila kujali ni mwanaume au mwanamke.

Hiyo inasaidia wengine wasirudie tabia hizo za kishenzi.
 
Hata Mimi ningekuwa yeye lazima nimsoteshe hata kwa sekunde tu lupango
 
Mimi nadhani kuikomesha tabia hii ni kumtenda aliyekutenda au aliyewatenda wengine alipokuwa madarakani na sio kuendeleza tabia kwa wapya.

Mfano, Hichilema ahakikishe Lungu anayapata machungu kulipa aliuofanya.

Au hapa kwetu mfano CCM inaondolewa madarakani, basi wale wote walio tesa watu kwa makusudi wakitumia madaraka na uchama wao waipate fresh bila kujali ni mwanaume au mwanamke.

Hiyo inasaidia wengine wasirudie tabia hizo za kishenzi.
You might be right, lazima kuwe na deterance of others from commiting atrocities when in power
 
You might be right, lazima kuwe na deterance of others from commiting atrocities when in power
Ukweli mimi hawa wa hapa wamenikifu hakuna mfano. Mtu mnyenyekevu hadi anakera kama Mbowe wana mbambikia kesi kama ya ugaidi?

Hawa watu wanajua jinsi Mbowe alivyoshiriki kuwafanya Wanachadema na wapinzani kuendesha siasa za amani na kutokuwa na visasi?

Zawadi yake ni kwenda kumlaza sakafuni, kutomleta mahakamani na yote waliyo mfanyia?

Hawa sio wa kuwaacha hivihivi wakati ukifika, hata Biblia imesema mtu akikupiga kibao kushoto mgeuzie na kulia. Mbona haijasemwa ukimgeuzia na kulia akikupiga unafanyaje?

Tafsiri yake ni kuwa huyo hajajifunza kuwa kakukosea ndio maana kakupiga tena kulia hivyo malizana naye.

Mungu sio wa viumbe wanyonge, ukiwa kwake we ni jasiri.
 
Kinacho tutesa Waafrika ni ubinafsi na kuto kujiamini. Wazungu waendelee tu kubarikiwa. Hakuna namna.
 
Ni wazi mgombea wa upinzani nchini Zambia atatangazwa mshindi.

My concern is: Historia inatukumbusha kuwa Hichilema aliwekwa ndani na Lungu kwa kumpa kesi ya kumbambikia ya Uhaini. Mahakama ikamweka huru.

Kwa akili za Waafrika tulivyolaaniwa, huyu mteule Hichilema atafanya hayo hayo kwa Wapinzani wake Mara akiapishwa.

It is a matter of some few days to come we will witness atrocities commanded by him against opposition as we see Samia "killing" Mbowe!
is why mkiwa na madaraka watendeeni mema wapinzani wenu. Unapomfanyia mtu ubaya, akija kufanikiwa usidhani atawaacha salama. ni wachache wenye moyo wa kusamehe.

Hii cycle of revenge inatesa sana viongozi wengi africa. wakitaka iishe waache kufanyiana hila. kuna leo na kesho
 
Wakati mwingine unawaza
Malawi na Zambia wamebadilisha vyama mara nyingi sana

Imewasaidia nini?
 
Waafrika kama watato wa baba mmoja na mama mbalimbali
 
Ni wazi mgombea wa upinzani nchini Zambia atatangazwa mshindi.

My concern is: Historia inatukumbusha kuwa Hichilema aliwekwa ndani na Lungu kwa kumpa kesi ya kumbambikia ya Uhaini. Mahakama ikamweka huru.

Kwa akili za Waafrika tulivyolaaniwa, huyu mteule Hichilema atafanya hayo hayo kwa Wapinzani wake Mara akiapishwa.

It is a matter of some few days to come we will witness atrocities commanded by him against opposition as we see Samia "killing" Mbowe!

Mleta mada elewa kuwa duniani kote tawala za binadamu zinaandamwa na hulka za ubinafsi. Ndio asili ya binadamu. Hata nchi kama Marekani (US) inayochukuliwa kama ngome ya demokrasia iko katika mapambano ya kudumu dhidi ya hulka zinazotishia uhai wa demokrasia huko. Mfano mzuri ni jinsi nchi hiyo ilivyokabiliana na uongozi na wafuasi wa aliyekuwa Rais, Donald Trump na vuguvugu lake la MAGA la kutaka kurejesha ukuu wa watu weupe huko US.

US iliasisiwa kwa mapambano yaliyohitimishwa miaka ya 1780 na kazi kubwa ya kuunda katiba makini na kuweka mifumo na taasisi imara zilnazohakikisha nchi haiendeshwi kwa kutegemea hulka za viongozi.

Hivyo usipoteze muda wala kuwa concerned na tabia ya Rais Hichilema huko Zambia. Kuwa concerned na kama Zambia wana katiba makini, mifumo bora na taasisi imara zisizompa Rais absolute power ya kufanya kila ujinga/uovu anaojisikia kuufanya. Kama mfumo ni imara hawezi kufanya huo ujinga unaowaza. Kama sio, lolote lawezekana.

Viongozi wabaya wanapenda sana kuwa na absolute power juu ya mihimili na taasisi zote nchini. Trump alikuwa anamuonea wivu Putin, a strong leader, respected by his people na kumponda Obama. Bahati nzuri, system ya US hailei ujinga.

Afrika tunafanya kosa kubwa sana la kutegemea kupata viongozi “watakatifu” modeli ya masihi, mitume, au malaika. Halafu sisi tuwakabidhi akili zetu watuendeshee nchi kwa “busara na hekima zao”. Yaani tuishi kwa fadhila na huruma zao. Unasikia kauli kama: “ikimpendeza Rais, anaweza kuagiza mshahara uongezwe kwa asilimia ...”

Huko Afrika ya Kusini, ANC walipoingia madarakani 1994, haikuchukua muda viongozi weusi, kwa tamaa zao, wakaanza harakati za ufisadi kwa kasi ya 4G. Ironically, mfumo wa utawala ulioasisiwa na makaburu, ukawafunga breki.

Tuitazame Zambia kwa undani. Hichilema ni mtu binafsi na ubinafsi wake. Sio mtakatifu fulani. Hoja muhimu ni je, nchi inamruhusu kufanya lolote analotaka? Mfano mzuri tunao hapa kwetu - sisi tunaosubiri lini masihi atashuka kuja kututawala.
 
Hizo ni hisia zako tu, pengine asimfanyie kama unavofikiria na badala yake akaomba ushirikiano kwake, sababu wazambia wameiva kidemokrasia sawa na wazungu.
trend in Africa has never changed anyway, we are speaking from history/past experience
 
Kama yule jamaa wa Angola alimgeuka aliyemuweka madarakani sembuse huyo Hikilema(mlemavu kwa baadhi ya makabila )
 
Ni wazi mgombea wa upinzani nchini Zambia atatangazwa mshindi.

My concern is: Historia inatukumbusha kuwa Hichilema aliwekwa ndani na Lungu kwa kumpa kesi ya kumbambikia ya Uhaini. Mahakama ikamweka huru.

Kwa akili za Waafrika tulivyolaaniwa, huyu mteule Hichilema atafanya hayo hayo kwa Wapinzani wake Mara akiapishwa.

It is a matter of some few days to come we will witness atrocities commanded by him against opposition as we see Samia "killing" Mbowe!
Oofcoz huwez kuusemea moyo Ila muda mwingne sisi waafrika tunashida Mahal, nikikumbuka mwai kibaki alivyokataa kuondka madarkan, yule wa ivory coast quattara naye hivyo hivyo aliingia kwa mbinde baada umoja was mataifa kuingilia lkn bado akafanya vilevile baada ya muda wake kumalizika akalazimisha kibaki.. du.. anything can happen Ila naenjoy Sana pale demokrasia inapochukua nafas
 
Mleta mada elewa kuwa duniani kote tawala za binadamu zinaandamwa na hulka za ubinafsi. Ndio asili ya binadamu. Hata nchi kama Marekani (US) inayochukuliwa kama ngome ya demokrasia iko katika mapambano ya kudumu dhidi ya hulka zinazotishia uhai wa demokrasia huko. Mfano mzuri ni jinsi nchi hiyo ilivyokabiliana na uongozi na wafuasi wa aliyekuwa Rais, Donald Trump na vuguvugu lake la MAGA la kutaka kurejesha ukuu wa watu weupe huko US.

US iliasisiwa kwa mapambano yaliyohitimishwa miaka ya 1780 na kazi kubwa ya kuunda katiba makini na kuweka mifumo na taasisi imara zilnazohakikisha nchi haiendeshwi kwa kutegemea hulka za viongozi.

Hivyo usipoteze muda wala kuwa concerned na tabia ya Rais Hichilema huko Zambia. Kuwa concerned na kama Zambia wana katiba makini, mifumo bora na taasisi imara zisizompa Rais absolute power ya kufanya kila ujinga/uovu anaojisikia kuufanya. Kama mfumo ni imara hawezi kufanya huo ujinga unaowaza. Kama sio, lolote lawezekana.

Viongozi wabaya wanapenda sana kuwa na absolute power juu ya mihimili na taasisi zote nchini. Trump alikuwa anamuonea wivu Putin, a strong leader, respected by his people na kumponda Obama. Bahati nzuri, system ya US hailei ujinga.

Afrika tunafanya kosa kubwa sana la kutegemea kupata viongozi “watakatifu” modeli ya masihi, mitume, au malaika. Halafu sisi tuwakabidhi akili zetu watuendeshee nchi kwa “busara na hekima zao”. Yaani tuishi kwa fadhila na huruma zao. Unasikia kauli kama: “ikimpendeza Rais, anaweza kuagiza mshahara uongezwe kwa asilimia ...”

Huko Afrika ya Kusini, ANC walipoingia madarakani 1994, haikuchukua muda viongozi weusi, kwa tamaa zao, wakaanza harakati za ufisadi kwa kasi ya 4G. Ironically, mfumo wa utawala ulioasisiwa na makaburu, ukawafunga breki.

Tuitazame Zambia kwa undani. Hichilema ni mtu binafsi na ubinafsi wake. Sio mtakatifu fulani. Hoja muhimu ni je, nchi inamruhusu kufanya lolote analotaka? Mfano mzuri tunao hapa kwetu - sisi tunaosubiri lini masihi atashuka kuja kututawala.
Umeandika vema sana. Bado andiko langu lina hold water in the sense kwamba, Je Hichilema ataimarisha mifumo bora ya democrasia? ... bunge, mahakama, katiba, sheria kandamizi etc etc , NGO or civil societies and the like?
Ataweza kutunga sheria/ktiba Kumdhibiti rais au kiongozi yeyote asiwe juu ya sheria na katiba kama lvyo hapa? Ana uthubutu wa kurekebisha mifumo iweze kumdhibiti yeye?
 
Back
Top Bottom