Waafrika wanamtamani Rais Magufuli kiuchumi lakini sio wazungu

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Waafrika popote walipo wanaokwerwa na wizi na uporaji wa mali zao unaofanywa na watawala wao wangefurahia wangekuwa na rais kama wa kwetu, JPM ambae kiuchumi hana mpinzani chini ya jangwa la Sahara Kwa sasa. Lakini wazungu kamwe huwa hawataki viongozi wa Africa wa aina hii.
Wazungu wanakumbatia maslahi yao tu Afrika basi bila kujali utawala Bora wala democracy za nchi hizo,

Siku yoyote ukisikia wazungu wanamyooshea kidole kiongozi wa Afrika Kwa lolote na chochote ujue kwamba kiongozi yuko sahihi Kwa hilo analolifanya kwa nchi na watu wake lakini sio sahihi kwa maslahi yao.

Mfano, Nyerere alitenda mengi mema Kwa watu wake na Africa lakini wazungu walimpenda Mandela kuliko Nyerere.

Walimpenda Moboutu, Kamuzu, ngwema lakini sio Nyerere, Kaunda, Lumumba, Nkwame, Gadaffi, Maduro, edogan, Saadam, NK.

Kelele zao ni dalili za usahihi wa kiongozi wa Africa Kwa taifa lake kiuchumi. Tusiogope.
 


Niwewe tu wa BRN
 
Wazungu haohao wanaokupa misaada au wazungu gani??
Wewe kumbe hujui kabisa. Wazungu hawana kitu cha bure hata kidooogo. Kila wanachokupa kina sababu na maslahi yao. Usisahau Ulaya na Marekani zimejengwa na mali kutoka mabara mengine na watumwa. Walituibia na wanaendelea kutuibia pia hadi kesho
 
Kulinganisha akili za Sokwe na mleta mada ni kumdhalilisha sokwe!....huyu akili yake bora Funza!
 
Hata kama maisha yetu yatakuwa mabaya chini ya JPM itakuwa sehemu tu ya uovu wa wazungu haohao ambao wamepania kutuachia mashimo na kuzoa madini yetu yote kwenda kwao. Hata kilichomponza Mugabe, Gadaffi, Saadam, Maduro na wengine no kuzikinga rasilimali zao zisiporwe. Wewe naona uko tayari mzungu alale na mkeo mladi tu maisha yako ya saafi Kwa fidia na misaada anayokupa.
Wewe akili yako ni afadhali ya wale wasiokuwa na akili kabisa, maana hujitambui.

Mnadhani uchumi utajengwa Kwa hisani za watu wengine, loh
 
Jana nilikuwa naangalia Taarifa ya habari ya hapa nyumbani TBC ni aibu.

Saa tatu nikaja kuangalia ya nchi nyingine nikasema Mungu ijalie nchi yangu.
 
Kulinganisha akili za Sokwe na mleta mada ni kumdhalilisha sokwe!....huyu akili yake bora Funza!
Kaskazini corridor syndrome. Mtapata taabu Sana.

Wako watu maisha yao yanakwenda Kwa kujikomba Kwa wazungu. Ukienda Ulaya na Marekani wamejaa huko wanafanyishwa kazi na wazungu, wanajenga taifa la wazungu Kwa taaluma zinazohitajika hata hapa nchi. Eti kisa hela hela hela hela hela. Uko tayari utiwe kidole popote mladi tu update hela. Watu kama nyinyinyi hamna tofauti na Mangungo wa enzi zile.

Mara nyingi watu kama nyinyinyi ni wale ambao babu na baba zenu walikuwa watumishi kwenye mashamba, majumba, na makanisa ya wazungu. Wanaomuona mzungu Kwa jicho na moyo wa Bwana mkubwa na yeye mtwana
 
Wewe kumbe hujui kabisa. Wazungu hawana kitu cha bure hata kidooogo. Kila wanachokupa kina sababu na maslahi yao. Usisahau Ulaya na Marekani zimejengwa na mali kutoka mabara mengine na watumwa. Walituibia na wanaendelea kutuibia pia hadi kesho
Sasa kataa hiyo misaada juha wewe tuone
 
Nina mashaka na kiungo unachotumia kufikiri (Nahisi si bongo, pengine Tumbo).
Unawezaje kuwasema vibaya wazungu wakati ndio wanaowapa misaada na hata budget yetu tunakadiria kwa kutegemea ruzuku zao?

Kama Magufuli aliweza kujitapa kuwa nchi tutaindesha wenyewe bila kutegemea wahisani na tena akaenda mbali zaidi kwa kusema "Nataka Tanzania iwe Donor country" na mpaka sasa ni zero....tena juzi kapokea mabilioni ya msaada kutoka kwa malkia, Leo hii unaongea pumba hizo....wee sema Marais wa Afrika wakishajulikana propaganda zao wanaanza kusingizia wazungu eti wachonganishi wakati wanaambiwa ukweli....

Badilika kijana acha uzwazwa!
 
Wazungu haohao wanaokupa misaada au wazungu gani??
Yes, hao hao wanaotupa msaada thamani ya thumni wanazoiba kwa kukiuka mikataba na kwa kutumia mikataba mibovu inayoandaliwa na wanasiasa wasio wazalendo. Jitafakari acha ushabiki, support your president.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

BRN wakuhurumiwa nyinyi, hamjielewi
 
Sio msaada bali ni sehemu tu ya dividend ya mali (mkonge, madini, kahawa, chai, watumwa) zetu walizotuiibia wakati wa ukoloni na kuwekeza kwao. Kama ukiwa na mawazo hayo kuwa wanatusaidia hatutafika mbali. Wanachotakiwa wao waache kutubia tena na waendeshe biashara kwa usawa na haki kati ya sisi na wao ili masoko ya pande mbili yapenyeke kwa wote.
 
Magufuli huyu aliepiga bei na kuhonga nyumba za serikali, Bilioni kadhaa kutoweka wizara ya ujenzi, bila kusahau kivuko cha Mv DAR ES SALAAM Kupida pesa za seikali na kuwakabidhi Wajeshi . You are having a laugh
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…