Waafrika wanathamini madaraka kuliko elimu na ufahamu

Waafrika wanathamini madaraka kuliko elimu na ufahamu

Storywriter

Senior Member
Joined
Jan 8, 2023
Posts
175
Reaction score
389
Watu wenye maarifa, elimu na ufahamu hawapewi kipaumbele sana hapa kwetu. Hawaheshimiwi, wala kuthaminiwa sana. Hii imekuwa moja wapo ya sababu za kurudisha maendeleo nyuma.

Wapo watu waliojitolea maisha yao yote kwa ajili ya kuisaidia jamii, kwa mfano madakatari bingwa wanaotibu magonjwa ya kufisha, wataalamu wa sayansi ya kilimo wanaotengeneza mbegu za kisasa, walimu na wahadhiri wakubwa wanaofanya tafiti za kisomi kwa manufaa ya jamii, wataalamu wa sayansi ya mawasiliano wanaotengeze mifumo ya ki-electroniki kwa ajili ya shughuli za kupeleka habari, kukusanya, kutunza na kusambaza data na taarifa.

Tumewapa kipaumbele sana wapiga porojo. Watu wasio na ufahamu na maarifa ya kutosha namna dunia inavyojiendesha na mifumo yake. Kuna wakati eti hawa wapiga porojo wamekuwa na amri zidi ya watalaamu na mabingwa

Utakuta eti diwani wa kata anayejua kusoma na kuandika tu anamkataa daktari aliyekaa darasani miaka 5. Utasikia "sitaki huyu dakatari afanye kazi kwenye kata yangu". Naishauri Serikali isikubali kabisa upuuzi wa hawa wapiga porojo.

Tukitaka kutoka hapa tulipo kama taifa lazima tuheshimu wataalamu. Tukatae kuendekeza wanasiasa uchwara wasio na tija yoyote zaidi ya majungu na fitina.
 
Watu wenye maarifa, elimu na ufahamu hawapewi kipaumbele sana hapa kwetu. Hawaheshimiwi, wala kuthaminiwa sana. Hii imekuwa moja wapo ya sababu za kurudisha maendeleo nyuma.
ma tuheshimu wataalamu. Tukatae kuendekeza wanasiasa uchwara wasio na tija yoyote zaidi ya majungu na fitina.
Tatizo kubwa ni ccm
 
Watu wenye maarifa, elimu na ufahamu hawapewi kipaumbele sana hapa kwetu. Hawaheshimiwi, wala kuthaminiwa sana. Hii imekuwa moja wapo ya sababu za kurudisha maendeleo nyuma.

Wapo watu waliojitolea maisha yao yote kwa ajili ya kuisaidia jamii, kwa mfano madakatari bingwa wanaotibu magonjwa eshimu wataalamu. Tukatae kuendekeza wanasiasa uchwara wasio na tija yoyote zaidi ya majungu na fitina.
Umesahau, wanathamini uchawi na ushirikina.
 
Kwa sababu supposedly, and rightly so, ukiwa na madaraka Afrikkkka, unaweza kununua ^elimu^ & ^ufahamu^
 
Elimu na ufahamu havinunuliwi ni lazima ukae chini ujifunze.

Hebu na pesa zako pale Muhimbili ukanunue udaktari kama inawezekana. Pesa inaweza kununua madaraka siyo elimu na maarifa.
Kwani wewe hujaona utitiri wa madokta nchini? Mpaka na wenyewe wameanza kujishtukia yaani! Wake up!
 
Kwani wewe hujaona utitiri wa madokta nchini? Mpaka na wenyewe wameanza kujishtukia yaani! Wake up!
Kwa hiyo hao madaktari wamenunua udaktari?

Hizi ndio akili zinazoamini katika mambo ya shortcut. Yaani watu kama nyie hamuamini katika uhalali. Mnaamini ukiwa na pesa unaweza kupata chochote. Nataka nikiambie kuna vitu havinunuliwi kwa pesa. Hata kama utasema umevipata kwa pesa vitu hivyo vitakuwa fake tu. Yaani udaktari fake n.k
 
Kwa hiyo hao madaktari wamenunua udaktari?

Hizi ndio akili zinazoamini katika mambo ya shortcut. Yaani watu kama nyie hamuamini katika uhalali. Mnaamini ukiwa na pesa unaweza kupata chochote. Nataka nikiambie kuna vitu havinunuliwi kwa pesa. Hata kama utasema umevipata kwa pesa vitu hivyo vitakuwa fake tu. Yaani udaktari fake n.k
Pesa ni sabuni ya roho, wao wanakwambia. Wala siyo mimi. Ndiyo maana scholars wengi sana hudiriki kuomba ufadhili wa matajiri (walioupata kwa wizi, utapeli, uonevu, uchawi, rushwa, madawa ya kulevya, ujambazi, nk), ili wakamilishe masomo yao ya Falsafa ya Uadilifu na Miiko. Hahaha!
 
Ni aibu madaktari kutawalia tu na mwanasiasa. Inabidi waongozwe na mtu aliyebobea katika hiyo taaluma.
 
Pesa ni sabuni ya roho, wao wanakwambia. Wala siyo mimi. Ndiyo maana scholars wengi sana hudiriki kuomba ufadhili wa matajiri (walioupata kwa wizi, utapeli, uonevu, uchawi, rushwa, madawa ya kulevya, ujambazi, nk), ili wakamilishe masomo yao ya Falsafa ya Uadilifu na Miiko. Hahaha!
Lete hapa ushahidi wa haya unayayesema. Weka takwimu za scholars walisomeshwa kwa pesa za ujambazi.

Nimekuambia wewe ni miongoni mwa watu mnaoamini katika kufoji kila kitu. Upo mahali fulani si kwa uhalali bali rushwa na shortcut.

Maandishi yako yanaonesha jinsi ulivyo. Naomba nikuambie dunia haendeshwi na wajinga au ujinga. Ingawa wajinga hawakosekani pia.

Kama ujinga na wajinga wangekuwa wanaendesha dunia, basi haya maendeleo ya sayansi na teknolojia yaliyopo duniani leo tusingeyaona. Maana wajinga wanaamini katika fojali ,rushwa na shorcut.
 
Simply because ukiwa na madaraka (hatakama haujasoma), unauhakika wa kula mema ya dunia kuliko kuwa msomi na mwenye maarifa, bado utapigika kwasababu hauna madaraka.
 
Simply because ukiwa na madaraka (hatakama haujasoma), unauhakika wa kula mema ya dunia kuliko kuwa msomi na mwenye maarifa, bado utapigika kwasababu hauna madaraka.
Je unadhani hii iko saw a?

Je tufunge vyuo vyote ,halafu wote tuanze kugombania madaraka ya udiwani, ubunge na urais?
 
Je unadhani hii iko saw a?

Je tufunge vyuo vyote ,halafu wote tuanze kugombania madaraka ya udiwani, ubunge na urais?
Mkuu.... hii ikiwa sawa ama isiwe sawa, hakuna tunachoweza kubadilisha mimi na wewe. Huu ni mfumo/ni mtandao wa watu wenye nguvu
 
Lete hapa ushahidi wa haya unayayesema. Weka takwimu za scholars walisomeshwa kwa pesa za ujambazi.

Nimekuambia wewe ni miongoni mwa watu mnaoamini katika kufoji kila kitu. Upo mahali fulani si kwa uhalali bali rushwa na shortcut.

Maandishi yako yanaonesha jinsi ulivyo. Naomba nikuambie dunia haendeshwi na wajinga au ujinga. Ingawa wajinga hawakosekani pia.

Kama ujinga na wajinga wangekuwa wanaendesha dunia, basi haya maendeleo ya sayansi na teknolojia yaliyopo duniani leo tusingeyaona. Maana wajinga wanaamini katika fojali ,rushwa na shorcut.
Simply because ukiwa na madaraka (hatakama haujasoma), unauhakika wa kula mema ya dunia kuliko kuwa msomi na mwenye maarifa, bado utapigika kwasababu hauna madaraka.
 
Back
Top Bottom