DOKEZO Waajiriwa wa mwaka 2021 hospitali ya Manispaa ya Kahama hawajalipwa stahiki zao

DOKEZO Waajiriwa wa mwaka 2021 hospitali ya Manispaa ya Kahama hawajalipwa stahiki zao

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Joined
Jan 28, 2024
Posts
17
Reaction score
10
Kumekuwa na tatizo la ukosefu wa uwajibikaji na uwajibishwaji wa viongozi wa hospitali ya Manispaa ya Kahama mjini kwani kero ni nyingi wanazokumbana nazo wafanyakazi ikiwemo waajiriwa wapya wa mwaka 2021 pesa zao ambazo walipaswa kulipwa haki yao hawakupewa lakini kwenye salary sleep zao zinaonesha kuwa walilipwa na wapo wengi lakini wakienda benki kuomba statement pesa hazionekani lakini toka mwaka huo mpaka leo hawajalipwa pesa zao lakini kwasababu kumekuwa na mazingira ya vitisho wanaogopa kusema hivyo.

Tunaomba viongozi wa juu wanaohusika wafuatilie hili suala pesa za watumishi wapya hawa kwanini hawajalipwa na anayehusika kwanini hajachukuliwa hatua mpaka leo?

Je, kwa hali hii rushwa tutaweza kuidhibiti?

Tunaomba msaada ili watumishi hawa wapate stahiki zao na haki itendeke. Wanafanya kazi kubwa mnoo ya kuwahudumia wagonjwa na sio wao tu, nchi nzima wauguzi na madaktari wanafanya kazi kubwa lakini hakuna motisha.

Nina imani Serikali inafanya kazi yake kwa sehemu yake ipasavyo shida ni viongozi waliokasimiwa madaraka wanayatumia vibaya.
 
Labda mimi ndio sijaelewa, hao wafanyakazi wa mwaka 2021 hawajalipwa mshahara au pesa gani hiyo unayodai?
 
Labda mimi ndio sijaelewa, hao wafanyakazi wa mwaka 2021 hawajalipwa mshahara au pesa gani hiyo unayodai?
Na kweli afafanue vizuri. Na afafanue kwenye hizo "salary sleep" kama alivyoziita zaidi ya mshahara kuna kitu gani kingine kama stahiki ya mwajiriwa kinaweza kuandikwa kuwa kimelipwa wakati hakijalipwa.
 
Back
Top Bottom