MotoYaMbongo
JF-Expert Member
- Jan 7, 2008
- 2,146
- 886
Waalimu ndg zangu nawauliza ni kweli mlirudi kazini au abrakadabra na mazingaombwe mlioyafanya? Kwanza kabisa nauliza hivi kwa sababu sioni kabisa dalili za nyie kuwepo kazini kwani picha halisi tumeziona kwenye matokeo ya mitihani ya watoto wetu wa drs la saba japo serkali na yenyewe imecheza filamu ya namna yake kwamba ufaulu umeongezeka kwa asilimia 8.8 na wakati wamechagua wanafunzi waliopata alama chini ya nusu yaani alama 60 kati ya 250 huu si usanii na usaliti wa taifa letu?Sasa sijui serkali ina malengo gani na Watanzania? Sasa hapa nauliza wazazi ambao ni wananchi pia mna malengo gani na watoto pamoja serkali hii inayotupa dira ya namna hii, kwa waalimu wao walisharidhika na wanachokipata lakini je mko kazini kweli au ni mazingaombwe