Researcher
Senior Member
- Dec 15, 2010
- 187
- 48
Pamoja na kwamba haujakuwepo utafiti wa kina katika hili, nimejiridhisha kwamba hili limeanza kuwa tatizo sugu na kuna sababu ya kuliangalia swala hili kwa kina ili kunusuru elimu yetu.
Pengine kutokana na ufinyu wa kipato na mfumo duni wa ukaguzi, waalimu wengi haswa wale ambao ni degree holders wamekuwa wakishika ajira zaidi ya moja. Wakuu wa shule za serikali wanatambua na wanawapa ushirikiano walimu wao katika kushiriki utoro huu ambao unadhoofisha ubora wa elimu yetu. Mfumo wa ruhusa za kiofisi pamoja na uhamisho nao ni mgumu kiasi cha kuwafanya walimu wengine kujisomea kozi za full time bila kuwa na likizo na pia kufanya kuishi mbali na shule wanazofundisha.
Napendekeza swala hili liangaliwe na ikiwezekana serikali iboreshe maslahi ya walimu sambamba na kudhibiti uwajibikaji wao.
Nasisitiza tena kwamba wapo walimu wengi sana wenye ajira zaidi ya moja na swala hili lisipochukuliwa hatua tutazidi kuudidimiza mfumo wa elimu Tanzania!
Pengine kutokana na ufinyu wa kipato na mfumo duni wa ukaguzi, waalimu wengi haswa wale ambao ni degree holders wamekuwa wakishika ajira zaidi ya moja. Wakuu wa shule za serikali wanatambua na wanawapa ushirikiano walimu wao katika kushiriki utoro huu ambao unadhoofisha ubora wa elimu yetu. Mfumo wa ruhusa za kiofisi pamoja na uhamisho nao ni mgumu kiasi cha kuwafanya walimu wengine kujisomea kozi za full time bila kuwa na likizo na pia kufanya kuishi mbali na shule wanazofundisha.
Napendekeza swala hili liangaliwe na ikiwezekana serikali iboreshe maslahi ya walimu sambamba na kudhibiti uwajibikaji wao.
Nasisitiza tena kwamba wapo walimu wengi sana wenye ajira zaidi ya moja na swala hili lisipochukuliwa hatua tutazidi kuudidimiza mfumo wa elimu Tanzania!