waandishi wa magazeti...msituharibie lugha tafadhali

waandishi wa magazeti...msituharibie lugha tafadhali

Chujio

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2013
Posts
1,368
Reaction score
2,108
hili halijaanza jana wala juzi ila siku hizi imezidi mno na kuwa kero. tafadhali sana waandishi wa magazeti, naombeni mzigatie uandishi wa kiswahili fasaha na sahihi pasipo kukera wasomaji... unakuta mwandishi kabisa anaandika neno "razi" au "lazi" badala ya radhi kwenye gazeti linalosomwa na wengi.. au unakutana na lajisi, latiba kha! jamani, kiingereza tukosee basi hata kiswahili nacho? wahariri wa uandishi jamani angalieni hilo kabla ya kuchapisha habari rasmi, tunawasihi tu zingatieni matumizi na uandishi ulio sahihi wa lugha yetu, maana inaharibika kweli siku hizi.

ni hayo tu
 
Labda hawana wataalamu wa lugha huko katika vyumba vya habari. Inakera sana hii ishu.
 
Tatizo hapa ni adhari za lugha mama yaan lugha za makabila mf wakuria hutumia xana r hivyo hata kwenye l wanaweka r!jambo la msingi hapa ni kuhakikisha kwamba zile athari za lugha mama haziharibu kiswahili na hiyo ni xifa ya wataalamu wa lugha
 
...tatizo kiswaili hakijawaigi kusaminiwa,afu kiswaili kibovu ndo kinauza kitaa mazee...
 
Nasikitika sana kusikia redioni au kusoma gazetini mtu tena msomi akisema 'nyimbo' huku akiwa na maana ya 'wimbo'. Eti 'nyimbo' mpya ya msanii Juma Nature inapendwa!
 
...tatizo kiswaili hakijawaigi kusaminiwa,afu kiswaili kibovu ndo kinauza kitaa mazee...

Duuuh, bado tuna safari ndeeeefu!
Gefu, sasa umeandika nini hapo?
Hicho kinachozungumzwa naona wewe umekiivisha kabisa!
...kiswaili .... Hakijawaigi...... Kusaminiwa.... Afu...kitaa....
Mazee.....
Ulikuwa na nia ya kuandika kiswahili au unaandika ki-lugha ya kwenu??
 
Duuuh, bado tuna safari ndeeeefu!
Gefu, sasa umeandika nini hapo?
Hicho kinachozungumzwa naona wewe umekiivisha kabisa!
...kiswaili .... Hakijawaigi...... Kusaminiwa.... Afu...kitaa....
Mazee.....
Ulikuwa na nia ya kuandika kiswahili au unaandika ki-lugha ya kwenu??

...ni msisitzo wa halihalisi ya kitaa mazee, ukiona maandamano ya haki beba bango linalo elezea uovu usibebe bango la kusifia haki hautasaidia kurekebisha makosa husika, pamoja mazeee.....?? teh teheehe ....
 
Tatizo hapa ni adhari za lugha mama yaan lugha za makabila mf wakuria hutumia xana r hivyo hata kwenye l wanaweka r!jambo la msingi hapa ni kuhakikisha kwamba zile athari za lugha mama haziharibu kiswahili na hiyo ni xifa ya wataalamu wa lugha

na wewe acha kutumia x katika uandishi wako humu.
 
Asante sana mleta mada kwa kuibua jambo la waandishi kuharibu ligha. Pia miminishakumbana na tatizo la kutotumia herufi 'h' pale inapohitajika. Mathlan, mwandishi ataandika ataki badala ya hataki, ama uyo badala ya huyo nk.
 
Back
Top Bottom