Wabongo wasusia kesi ya Jack Cliff atokwa na chozi Kortini

Money Stunna

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2011
Posts
13,053
Reaction score
6,304
HATIMAYE modo maarufu Bongo, Jacqueline Fitzpatrick ‘Jack Patrick’ amepandishwa kortini kwa mara ya kwanza huko Macau nchini China, Aprili 10, mwaka huu kwa kukutwa na madawa ya kulevya tumboni aina ya heroin kete 57 au kilo 1.1 yakiwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni 223 huku ishu kubwa kwa muda wote aliokuwa mahakamani ikiwa ni kuangua kilio kila wakati.

Jack alipandishwa kwenye korti hiyo ikiwa ni mara yake ya kwanza tangu alipokamatwa na madawa ya kulevya ‘unga’ Desemba mwaka jana akitokea Bongo kupitia Thailand na kuingia nchini humo.
ILIKUWAJE?
Kwa mujibu wa chanzo chetu makini kilichopo Macau, Jack alifikia hatua hiyo dakika 15 baada ya kupanda kizimbani na kukutana na nyuso za Wachina tu zikimwangilia

“Yeye alijua angekuta Wabongo au hata watu weusi wakimpa kampani, lakini matokeo yake alikutana na sura za Wachina tu,” kilisema chanzo chetu.
Kikaendelea: “Unajua kwa kawaida mtu anapopanda kizimbani mara zote anafarijika sana endapo atawaona anaowafahamu, hasa ndugu zake ambao watafika kumtia moyo, sasa yeye hakulipata hilo.”
DAKIKA 10 ZATUMIKA KUMSOMEA MASHITAKA
Kuna madai kwamba, msoma mashitaka wa mahakama hiyo alitumia dakika 10 kutokana na taratibu za kisheria za huko huku akitakiwa kusema ndiyo au hapana tu kabla keshi hiyo kupigwa kalenda hadi Mei 23, mwaka huu

KUNA MADAI ALIZOMEWA
Chanzo hicho kiliendelea kudai kwamba, mbali na kukutana na upweke huo mahakamani, pia Jack alipata kisanga kingine pale baadhi ya raia wa nchi hiyo walipomzomea kwa sauti ya chini wakati akitoka kortini.
Inadaiwa kuwa, kwa Wachina kumzomea au kumsema vibaya mtu aliyedakwa na madawa ya kulevya ni kawaida kwani hakuna biashara, inapigwa vita nchini humo kama ya unga wakiamini unaangamiza nguvu kazi ya kizazi kijacho.
NDUGU WADAIWA KUMKATIA MAWASILIANO
Habari nyingine kutoka chanzo chetu zilidai kwamba, kwa sasa Jack amebaki yeye na Mungu wake baada ya nduguze waishio Bongo kumkatia mawasiliano kwa kile walichodai kuwa kitendo alichokifanya kimeiaibisha familia nzima.
“Unajua ndugu zake walikata mawasiliano kabisa? Nchi nzima au tuseme dunia nzima kilio ni jinsi vijana wanavyoharibika kwa madawa ya kulevya, sasa kule kubainika kwamba Jack alibeba unga tumboni kwenda kuuza kumeifanya familia kujisikia vibaya sana,” kiliongeza chanzo hicho kikiomba chondechonde kisitajwe gazetini.

KAMA ATARUDI BONGO SALAMA
Habari zaidi zinadai kwamba modo huyo ambaye pia ni Miss Ilala No 3, 2005, aliwahi kumwambia mshirika wake mmoja akiwa mahabusu kwamba, kama atabahatika kurejea Bongo salama,
atakwenda kupiga dua juu ya kaburi la mama yake ili amsimamie katika kumwondolea nuksi kama siyo mabalaa. Baba wa Jack anadaiwa kuishi nje ya nchi.
TUJIKUMBUSHE
Jack alikamatwa Desemba 19, mwaka jana kwenye Uwanja wa Ndege wa Macau nchini China akitokea jijini Bangkok nchini Thailand kuelekea Guangzhou, Mji Mkuu wa Jimbo la Guangdong Kusini mwa China ambako ilidaiwa ndiko alikokuwa anafikisha unga huo.
Ilidaiwa kuwa miongoni mwa mambo yaliyochangia kukamatwa kwake ni kuonesha uso wenye uchovu, kuanza kuwa na hali mbaya ya mwili, kushindwa kujibu maswali vizuri na hati yake ya kusafiria, yaani ‘passport’ kukutwa imegongwa mihuri ya kuingia nchini humo kila mara jambo ambalo wakaguzi waliliona si la kawaida kwa msichana kama yeye.
 
Mkuu kama kuna picha za Kortini zitupieni
 
Duuh! hawa Dada zetu ifike mahali watulie..Fanyeni kazi..

Aaaah 🙁
 
Afu huyo Duu -------- sana!
Hivi kukamatwa na madawa nako ni Nuksi?

Si utaira wake yeye mwenyewe kupenda Maisha Mtelezo !
Na kugeuzwa punda

Bora angetulia tu bongo ajigongeshe gongeshe kwa wanaume !
Mbona akina Wema sepetu, Kajala n.k ndo staili wanazotumia kuishi hapa mjini !

Mi naona China Wakimnyonga huyo afu afuatie na Masogange ajipitishe China nae akanyongwe mana anajifanya anaishia south Africa ! Tu

Afu bado Domo nae tushamjua pamoja na wengine ambao majina tunayo kapuni !
Watoto wa vibosile ! Wanawatumia akina Jack, Domo kama punda wao ! Daaaa

Inusulu Tanzania !
Jacky Cliff akinyongwa sababu hasa ni kupenda Maisha Mtelezo !

snipa
 
Last edited by a moderator:
wanapenda maisha ya dezo acha wapate fedheha labda watajifinza
 
Akichomoka huko co tu kwenda kaburini, aje pande Za songea huku kuna kubeba sembe poa co sembe la mawazo!!!


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Pole yake.....aubebe msalaba wake tu mana kila mtu atauchukua msalaba wake mwenyewe siku ikifika....
 
Wapi papaa Kinje na Miraji nakati ya muji. Ebu fanyeni mambo yetu yalee kama ya sauz mbebz wa ukwee atokepo...
 
kunyongwa lazima hadi ndugu washajua atoki
 
vinakuaga na dharau hivi ukikutananavyo mjini analia nn sasa
 
*****, mashauzi yote yamepaa.Mkiambiwa fanyeni kazi, kazi msingi wa maisha hamtaki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…