Wabunge:Laki si pesa tumekubali,vipi kanuni mbona hamziweki wazi mpate ushauri?

Wabunge:Laki si pesa tumekubali,vipi kanuni mbona hamziweki wazi mpate ushauri?

kibaravumba

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
6,634
Reaction score
7,015
Tunajua sasa suala la posho ilikuwa mpango mahsusi wa wasiolitakia mema taifa kututoa kwenye mjadala wa msingi ambapo sasa ni kanuni za kuendesha bunge maalum la katiba.Sisi wananchi wa Tanzania,tuliokubali muwe wawakilishi wetu huko Bungeni,tunataka kujua kanuni hizo zikoje kabla hamjazijadili,ili tutoe maoni yetu ikiwa ni kuboresha na kuweka wazi kila hatua ili mjadala uwe na baraka zote.Tunasikia tu kuna njama za kutaka kuweka ukiritimba na kufanya mambo mengine kama siri.Tusingependa mambo haya yatokee na kulazimisha njia za mashinikizo ambazo mara nyingi hugharimu muda na hata maisha ya watu.Mungu ibariki Tanzania

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom