kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Wajumbe wa bunge la katiba mlioko Dodoma usiwe kama maroboti yanayopangiwa na mtengenezaji nini cha kutenda bila kufikiri hata kidogo. Sisi wananchi tunafahamu na tunafuatilia yanayotendeka huko mjengoni kuhusu mjadala wa katiba, hivyo tunajua ni wajumbe gani wako kama maroboti yaliyoamriwa cha kufikiri na kutenda ndani ya bunge. Maana hata Nyerere alisemaga kuwa kama mtu mwenye akili timamu atapewa usharauri wa kijinga na mtu mwenye akili timamu halafu akaukubali na kuutekeleza kama ulivyo, basi mtoa ushauri atakuwa anamfanya mjinga mpokea ushauri huo.
Hivi mjumbe wa bunge la katiba mwenye akili timamu utakubalije kupewa ushauri/msimano wa kijinga na mtu mwingine mwenye akili timamu kama wewe na kuukubali?
Jiulize mwenyewe maswali yafuatayo:
1. Ushauri/msimamo unaopewa una maslahi gani kwa watu wa Tanganyika na Zanzibar?
2. Katiba tuliyonayo ilitungwa na wakina nani? na walikuwa wangapi?
3. Rasimu ya katiba mpya imetungwa na wakina nani? na walikuwa wangapi?
4. Kura ya wazi au kura ya siri zitasababisha matokeo gani ndani ya jamii? amani, chuki, upendo, mshikamano uadui uwadui kati ya mtu na mtu?
5. Wewe unadhani watanzania (bara na visiwani) wanataka katiba ya namna gani? na kama wasipoipata katiba wanayoitaka kwasababu yako na ujanja ujanja unadhani matokeo yake kwa miaka 50 mingine ijayo yatakuwaje? manung'uniko, furaha, kupendana, kuchukiana, uchumi kukua, uchumi kudorora, ugaidi, utulivu au nini? taja ___
Kuna wajumbe hapo wako kama maroboti leo hii mwenyekiti wa kundi lao akigeuka na akisema fanya hivi atafanya hivyohivyo bila kuhoji kama ndondocha.
Kwani shida yenu hasa maroboti ni nini? madaraka, woga, mali, heshima, kufa, kunyang'anywa au nini? taja_____
Fanya kazi kama wewe ili nchi iwe kama vile unavyotaka iwe
Hivi mjumbe wa bunge la katiba mwenye akili timamu utakubalije kupewa ushauri/msimano wa kijinga na mtu mwingine mwenye akili timamu kama wewe na kuukubali?
Jiulize mwenyewe maswali yafuatayo:
1. Ushauri/msimamo unaopewa una maslahi gani kwa watu wa Tanganyika na Zanzibar?
2. Katiba tuliyonayo ilitungwa na wakina nani? na walikuwa wangapi?
3. Rasimu ya katiba mpya imetungwa na wakina nani? na walikuwa wangapi?
4. Kura ya wazi au kura ya siri zitasababisha matokeo gani ndani ya jamii? amani, chuki, upendo, mshikamano uadui uwadui kati ya mtu na mtu?
5. Wewe unadhani watanzania (bara na visiwani) wanataka katiba ya namna gani? na kama wasipoipata katiba wanayoitaka kwasababu yako na ujanja ujanja unadhani matokeo yake kwa miaka 50 mingine ijayo yatakuwaje? manung'uniko, furaha, kupendana, kuchukiana, uchumi kukua, uchumi kudorora, ugaidi, utulivu au nini? taja ___
Kuna wajumbe hapo wako kama maroboti leo hii mwenyekiti wa kundi lao akigeuka na akisema fanya hivi atafanya hivyohivyo bila kuhoji kama ndondocha.
Kwani shida yenu hasa maroboti ni nini? madaraka, woga, mali, heshima, kufa, kunyang'anywa au nini? taja_____
Fanya kazi kama wewe ili nchi iwe kama vile unavyotaka iwe