Leak
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 52,916
- 43,505
Ina sikitisha sana kuona wabunge wetu pamoja na wale wateuliwa wamemua kuligeuza bunge hili maalum kama soko.
Kwakweli yeyote aliyepata nafasi ya kutazama hata kidogo mjadala wa bunge maalum atakubaliana nami kuwa wabunge wetu wameligeuza bunge hili maalum kama soko ndio maana bunge hili limekuwa sehemu ya kelele, uropokaji na kuzunguka zunguka kama sokoni.
Wengi tulitegemea bunge hili maalum lingekuwa la utulivu na kusikilizana na wabunge wetu wangetumia hekima na busara zaidi katika mijadala yote, lakini kinyume chake tuna shuhudia watu kuropoka, kuzunguka zunguka bungeni,kupiga kelele wakati wengine wakichangia. Kwakweli wabunge wetu wote wana tutia aibu kabisa wamekuwa kama watoto wadogo.
Pengine ni kwa sababu Mwenyekiti wa muda amekuwa mpole sana na anatumia busara sana na kwakweli wabunge wanamchosha sana na bila buasra anazo tumia Mwenye kiti wa muda wa bunge maalum basi hali ingekuwa mbaya zaidi ya hii ninayo iona.
Hakika kama bunge hili maalum litaendelea kwa namna hii lazima tukubali kuwa muda ulio tengwa hauto tosha kabisa.
Wabunge wetu wameshindwa kabisa kumheshimu Mwenye kiti wa muda ndio maana wengine wanagoma kukaa hata wanapo ambiwa kukaa chini katika hili nimesikitishwa sana kuna mbunge aliambiwa akae chini aka kataa na kuanza kupiga kelele kama mtoto,Mwenye kiti alitumia busara sana kumpuuza,
Ni vyema Wajumbe wote wa bunge maalum wakajua kabisa tumewatuma wakajadiliane hili kutupatia katiba mpya nasi kwenda kupiga kelele na kuzunguka ndani ya bunge na wengine wakitoka nje na kuingia hadi ni vigumu kujua kama mjadala unaendelea maana kila mtu anafanya lake.
Kwakweli yeyote aliyepata nafasi ya kutazama hata kidogo mjadala wa bunge maalum atakubaliana nami kuwa wabunge wetu wameligeuza bunge hili maalum kama soko ndio maana bunge hili limekuwa sehemu ya kelele, uropokaji na kuzunguka zunguka kama sokoni.
Wengi tulitegemea bunge hili maalum lingekuwa la utulivu na kusikilizana na wabunge wetu wangetumia hekima na busara zaidi katika mijadala yote, lakini kinyume chake tuna shuhudia watu kuropoka, kuzunguka zunguka bungeni,kupiga kelele wakati wengine wakichangia. Kwakweli wabunge wetu wote wana tutia aibu kabisa wamekuwa kama watoto wadogo.
Pengine ni kwa sababu Mwenyekiti wa muda amekuwa mpole sana na anatumia busara sana na kwakweli wabunge wanamchosha sana na bila buasra anazo tumia Mwenye kiti wa muda wa bunge maalum basi hali ingekuwa mbaya zaidi ya hii ninayo iona.
Hakika kama bunge hili maalum litaendelea kwa namna hii lazima tukubali kuwa muda ulio tengwa hauto tosha kabisa.
Wabunge wetu wameshindwa kabisa kumheshimu Mwenye kiti wa muda ndio maana wengine wanagoma kukaa hata wanapo ambiwa kukaa chini katika hili nimesikitishwa sana kuna mbunge aliambiwa akae chini aka kataa na kuanza kupiga kelele kama mtoto,Mwenye kiti alitumia busara sana kumpuuza,
Ni vyema Wajumbe wote wa bunge maalum wakajua kabisa tumewatuma wakajadiliane hili kutupatia katiba mpya nasi kwenda kupiga kelele na kuzunguka ndani ya bunge na wengine wakitoka nje na kuingia hadi ni vigumu kujua kama mjadala unaendelea maana kila mtu anafanya lake.