Wabunge wa CCM wafunga barabara na kuzuia mkondo wa maji hali inayowasababishia wananchi kupata mafuriko

Wabunge wa CCM wafunga barabara na kuzuia mkondo wa maji hali inayowasababishia wananchi kupata mafuriko

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Wabunge wastaafu na wale watarajiwa wa CCM wamejianzishia mtaa wao huko Ununio na kuuita Bunge Btreet, miongoni mwao ni Mzee Kimiti, Mh. Foya wa Hai, Mh. Adam wa Muleba na Mh. Kippi anayetarajia kugombea Kawe.

Cha kusikitisha wabunge hawa wamefunga barabara na kuzuia mkondo wa maji hali iliyopelekea eneo lote la mtaa wa Mombo kujaa maji kwa takribani miezi mitatu sasa.Wananchi wa eneo hilo wamemwendea diwani wa Kunduchi Mh. Urio ili awasaidie lakini awali Urio alidai hao wabunge ni mabosi wake ila atatafuta namna " nzuri" ya kuongea nao.

Baada ya kuongea nao serikali ya mtaa iliagiza wananchi wachangie sh 50,000 kila nyumba ili ujengwe mtaro lakini baada ya fedha kuchangwa diwani hapatikani wala hapokei simu.

Wananchi hao wamedai kuwa mambo ya UONEZI, dhuluma na unyanyasaji kama hayo ndio huwatia hasira na kuamua kuwachagua wapinzani.

Hadi sasa inaelezwa mafuriko hayo yamesababisha kifo cha mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Makaranga aliyefia ndani ya nyumba kwa kukosa msaada.

NB: Mh. Diwani Urio najua unapita humu nenda katatue kero za wapiga kura wako

CC: RC Makonda

CC: H. Mdee (MB)

Maendeleo hayana vyama
 
Mods nimeomba heading isomeke : Wabunge wa CCM wafunga barabara na kuzuia mkondo wa maji hali inayowasababishia wananchi kupata mafuriko!
 
Hapo umemtag Halima Mdee, she will never do anything, ni sawa tu na HAKUNA. As mkazi wa Goba, I have given up on her as mwakilishi wangu.
 
Hapo umemtag Halima Mdee, she will never do anything, ni sawa tu na HAKUNA. As mkazi wa Goba, I have given up on her as mwakilishi wangu.
Hata huko Ununio wanadai haonekani kabisa lakini nina imani RC Makonda atawasaidia maana analijua eneo husika kwani wananchi wanadai aliwahi kwenda kubomoa ukuta uliojengwa na mbunge wa Kibaha mh Koka na kuzuia barabara.
 
Mr urio kafanya yake

Sent from my Infinix X624 using Tapatalk
 
Mods nimeomba heading isomeke : Wabunge wa CCM wafunga barabara na kuzuia mkondo wa maji hali inayowasababishia wananchi kupata mafuriko!
Kimiti ni mbunge wa ccm jimbo gani mkuu? Huyu zama zake bado zipo tu?
 
Wabunge wastaafu na wale watarajiwa wa CCM wamejianzishia mtaa wao huko Ununio na kuuita Bunge Btreet, miongoni mwao ni Mzee Kimiti, Mh. Foya wa Hai, Mh. Adam wa Muleba na Mh. Kippi anayetarajia kugombea Kawe.

Cha kusikitisha wabunge hawa wamefunga barabara na kuzuia mkondo wa maji hali iliyopelekea eneo lote la mtaa wa Mombo kujaa maji kwa takribani miezi mitatu sasa.Wananchi wa eneo hilo wamemwendea diwani wa Kunduchi Mh. Urio ili awasaidie lakini awali Urio alidai hao wabunge ni mabosi wake ila atatafuta namna " nzuri" ya kuongea nao.

Baada ya kuongea nao serikali ya mtaa iliagiza wananchi wachangie sh 50,000 kila nyumba ili ujengwe mtaro lakini baada ya fedha kuchangwa diwani hapatikani wala hapokei simu.

Wananchi hao wamedai kuwa mambo ya UONEZI, dhuluma na unyanyasaji kama hayo ndio huwatia hasira na kuamua kuwachagua wapinzani.

Hadi sasa inaelezwa mafuriko hayo yamesababisha kifo cha mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Makaranga aliyefia ndani ya nyumba kwa kukosa msaada.

NB: Mh. Diwani Urio najua unapita humu nenda katatue kero za wapiga kura wako

CC: RC Makonda

CC: H. Mdee (MB)

Maendeleo hayana vyama
Hata picha umeshindwa kuweka ili tuone?
 
Back
Top Bottom