CCM ilipoteza kule kuaminika kabla ya uchaguzi wa 2015, hivyo uwepo wa Lowassa kama mgombea wa upinzani ukaonekana ni wa muhimu sana.
Iwapo Magufuli angekuwa rais mwaka ule kuelekea uchaguzi mkuu na akawa ni mtendaji kama alivyo sasa huyo Lowassa asingepata hata nusu ya kura alizozipata.
Udhaifu wa CCM ile ndio ulikuwa uimara wa Lowassa yule.