Wabunge wataka makali bei ya umeme ipungue

Wabunge wataka makali bei ya umeme ipungue

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274
Wabunge wameitaka Serikali kukokotoa upya bei ya umeme baada ya mradi wa kufua nishati hiyo wa Julius Nyerere (JNHPP) kukamilika ili kumpa nafuu Mtanzania.

Akiuliza swali la nyongeza bungeni leo Agosti 30, 2024, Mbunge wa Lupa, Masache Kasaka amesema mradi wa JNHPP umeanza uzalishaji umeme wa kutosha na kuna wa ziada.

Kutokana na hilo amehoji, “je, Serikali haioni haja ya kupitie upya ukokotoaji wa bei za uniti na baadaye kushusha bei ili kuleta nafuu kwa Mtanzania?”

Soma Pia: Nashauri Serikali kupunguza bei ya umeme kuchochea shughuli za kiuchumi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga katika majibu ya swali hilo amesema gharama za umeme si za uzalishaji peke yake, bali zinahusisha za usambazaji, usafirishaji na uwekezaji.

Hata hivyo, amesema kwa kuangalia bei za nishati hiyo katika nchi nyingine za Afrika Mashariki, Tanzania ina bei ya chini.


 
Bei ya umeme ishushwe ila sio kisa JNPP,
tutazame gharama ya uendeshaji mitambo pia
 
Kama hawata shusha bei za umeme na gesi wasahau huu uoto wa kijani, miti itakatwa km vita ya majimaji.
 
Hivi umaalum wa wafanyakazi wa Tanesco kupata umeme mwingi pindi wanunuapo ni upi tofauti na hawa wazindakaya wengine?
 
Hivi umaalum wa wafanyakazi wa Tanesco kupata umeme mwingi pindi wanunuapo ni upi tofauti na hawa wazindakaya wengine?
Kumbe wana special package tofauti na sisi walamba viatu
 
Wabunge wameitaka Serikali kukokotoa upya bei ya umeme baada ya mradi wa kufua nishati hiyo wa Julius Nyerere (JNHPP) kukamilika ili kumpa nafuu Mtanzania.

Akiuliza swali la nyongeza bungeni leo Agosti 30, 2024, Mbunge wa Lupa, Masache Kasaka amesema mradi wa JNHPP umeanza uzalishaji umeme wa kutosha na kuna wa ziada.

Kutokana na hilo amehoji, “je, Serikali haioni haja ya kupitie upya ukokotoaji wa bei za uniti na baadaye kushusha bei ili kuleta nafuu kwa Mtanzania?”

Soma Pia: Nashauri Serikali kupunguza bei ya umeme kuchochea shughuli za kiuchumi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga katika majibu ya swali hilo amesema gharama za umeme si za uzalishaji peke yake, bali zinahusisha za usambazaji, usafirishaji na uwekezaji.

Hata hivyo, amesema kwa kuangalia bei za nishati hiyo katika nchi nyingine za Afrika Mashariki, Tanzania ina bei ya chini.


Uzalishaji ni asilimia ngapi ya jumla ya gharama zote? Basi washushe kwa kiwango kile kile kwa kadri ya share ya uzalishaji katika gharama jumla
 
Mimi nashauri serikali ipandishe bei ya umeme iwe mara tatu ya bei ya sasa.
Na ikiwapendeza, serikali iongeze kodi ya electricity levy kwa kiwango cha 20%.
Watanzania wana hela, we angalia magari yaliyo barabarani yalivyo mengi na yote ni namba E tu.
Ambaye ataona bei ya umeme ni kubwa ahamie Burundi
 
Mimi nashauri serikali ipandishe bei ya umeme iwe mara tatu ya bei ya sasa.
Na ikiwapendeza, serikali iongeze kodi ya electricity levy kwa kiwango cha 20%.
Watanzania wana hela, we angalia magari yaliyo barabarani yalivyo mengi na yote ni namba E tu.
Ambaye ataona bei ya umeme ni kubwa ahamie Burundi
Namba E lakini ni second hand kutoka Japan [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
 
Back
Top Bottom