Wachagga na mila za kufukua maiti

Wachagga na mila za kufukua maiti

WilsonKaisary

JF-Expert Member
Joined
Apr 4, 2017
Posts
392
Reaction score
949
IMG_20200620_151210.jpg

Je, umewahi kusikia kuwa wachaga pindi wapendwa wao wanapofariki basi baada ya muda fulani kupita huenda kufukua mabaki ya miili ya maiti wao kisha kuwahifadhi sehemu maalumu?

Kwanza kabsa nchi yetu imebarikiwa kwa kuwa na makabila tofauti tofauti ambayo yametofautiana katika mila na desturi, hivyo mila ya kabila moja huweza kuwa ni kitu cha kushangaza sana kwa kabila lingine. Leo nimekuletea jambo la tofauti kidogo linalowahusu wachaga.

IMG_20200620_150512.jpg

Tuanzie hapa wachaga wana mila ya kutofikisha msiba usiku yaan kwa mfano mtu kafariki dar atasafirishwa kwenda kilimanjaro ila ikiwa safari itakuwa ni ya usiku basi kabla ya kuingia kijiji au mahali msiba utakapozikwa basi watalala kijiji cha jirani ili msiba ukafike kesho asubuhi.

Wao kwao ni nadra sana msiba kufikisha usiku Inasemakana sababu zinazopelekea kufanya hivyo kwanza ni kuepusha kuzua taharuki kwa wafiwa na majirani kuanza kuomboleza mapema, na kupiga kelele haipendezi. Pili ni imani na mila kuwa mwili wa marehemu ukifika unatakiwa kwenda kuzikwa Moja kwa moja.

KUFUFUA WAFU
Vilevile jambo lingine linaloweza kuwa geni kwa makabila mengine lakini ni utamaduni wa wachaga hasa wa kilema mkoani kilimanjaro ni hili la kuwafufua wapendwa waliofariki kila inapotimia miaka 8 au 10 baada ya kuzikwa. Mila hiyo ina taratibu Zake za kufuata kabla ya kufikia hatua ya mwili kufukuliwa sehemu iliyokuwa umezikwa na kwenda kuwahifadh sehemu nyingine, kitendo hiki kimekuwa kikifuata utaratbu maalumu wa kimila na kisipofanywa inaaminika kuwa na madhara makubwa kwa ukoo hasa kusababisha kifo.

Hivyo baada ya Maiti kufikisha miaka 8 au 10 wanafamilia huandaa vitu vinavyohitaji kisha humuita mtaalamu au mtu mila awasaidie kwenye masuala ya kufukua kwani sio kila mtu anaweza kuifanya hiyo kazi.

UTARATIBU WA KUFUKUA
IMG_20200620_150637.jpg


Siku moja, kabla ya saa kumi alasiri mzee wa mila ataotesha jani la Sale pamoja na kumwaga pombe ya mbege juu ya kaburi ambalo mtu anatakiwa kufufuliwa. Kesho yake asubuhi mzee wa mila huenda kuangalia kama jani hilo limenyauka au laah!!, kama halijanyauka ni ishara ya kwamba ya kwamba wakifukua kaburi hilo watakuta mafuvu ya mhusika, basi hapo Huchinjwa mbuzi na kunena maneno yanayotakiwa kuzungumzwa wakati anamwaga damu katika kaburi.

IMG_20200620_150724.jpg


Kisha wanaukooo wanaanza kufukua kaburi huku akiwaelekeza vitu vya kufanya, shughuli ya kufukua huendelea huku akina mama wakiendelea na shamrashamra za kupika maana inakuwa ni sherehe Kubwa. Mara tu watakapoanza kuona mabaki ya marehemu basi watasitisha kila kitu hapo wanawake wataruhusiwa kusogolea eneo hilo na kupiga vigeregere, kisha huwpa chakula wanaukoo.

Kwakuwa kazi huchukua muda mrefu basi inabidi kula na kunywa. Baada ya vigeregere kumalizika fuvu la Mhusika huchukuliwa kuwekwa kwenye jani la sale kisha kuhifadhiwa ndani. Fuvu hilo likishahifadhiwa ndani ni ishara ya kuwa mtu huyo ni hai na ci mfu tena kwa imani za wachaga wa kilema. Kesho yake asubuh na mapema hulichukua fuvu hilo na kulipaka mafuta ya "msuka samli" na kisha Kulifanyia mila zingine. Mzee wa mila atalishika fuvu hilo kisha wanaukoo huja mmoja mmoja kulipaka mafuta fuvu hilo huku kila mmoja akiomba anachokihitaji.

IMG_20200620_145901.jpg


Baadaye ataungana na wanaukoo kwa idadi sawa ya jinsi na wataelekea sehemu ya kulihifadhi "mbuoni". Wakati wanaelekea.

Mbuoni, Masharti ni kuwa hawaruhusiwi kugeuka nyuma, hadi wanapofika sehemu wanapoweka fuvu hilo.
Inasemakana pia baadhi ya sababu kufanya hivyo ni kutokana na ufinyu wa ardhi hali inayosababisha kuendeleza mila hiyo tangu enzi za mababu na mababu.
 
Mila zao zinafana na mila za watu wa Madagascar,,,wenyeji ambao huitwa wa Malagasy,, ila zina tofauti kidogo,,,na wa Malagasy,, wao huwa mtu akifa hawaziki kabisa,,,,Bali maiti huwekwa kwenye kibanda maalum mfano wa nyumba,,ambayo hujengwa makaburini,,,,mtu anapokufa siku ya kwnz watu wanalia,,siku ya tatu baada ya kuwekwa huko kwnye kibanda ambacho kipo makaburini,,,mkuu wa mila ndy mwenye mamlaka ya kufunguwa na kufunga kibanda hicho,,,siku ya tatu hufunga mziki wa kufa mtu nyumbani kwa marehemu,,,huku watu wakinywa na kucheza mziki..na baada ya mwaka mmoja tangu mfu kufariki sherehe zinaamia makaburini ambapo mfu hubadilishwa nguo na wana family hucheza nae mziki .na kuzunguka nae mitaani,,..hivyo basi kila mwana family atapata nafasi ya kubeba mwili wa mpendwa wao na kucheza nae mziki,,sherehe hizo hazibagui mtoto wala mtu mzima mradi tu ni mwana family,,, na pia sherehe hizo zinahudhuriwa na watu mbalimbali,,, pia zinakuwa na maandalizi ya hali ya juu...na wanakwambiya ukiwa Madagascar ukizikwa ardhini ni kama vile huna ndugu au ni mtu dhalili kabisa,,na wanaamini kuwa bila kumfanyia mfu hizo sherehe za kumbadilisha nguo kila mwaka,, basi mfu anaweza kuwapa laana wana family.... Kutokana na Uzi wa mleta maada pengine wachaga na wamalagas ni asili moja..
 
Hii niliikuta,lakini jinsi dunia inavyobadilika desturi kama hizo zinaachwa na walio wengi maana wametangaziwa habari njema na watu wengi kuiamini injili..Watu wa Moshi sasa hivi wamebadilika sana..hata zile mbege wanazokunywaga wanadai ni ngera ta wana na nyingine nyingi zimeachwa, Kwa imani za kuwa wanaukoo wengine wanaanda sherehe za kifrimason ...halafu watu watakao kuja kusherekea baadhi yao wanachukuliwa nyota..Hivyo wamama wengi wamekua makini sku hizi..hawaendi kwenye sherehe za majumbani kama Kanisa halijaalikwa
 
Maisha ya mwanadamu yamegawanyika katika parts mbalimbali kulingana na tamaduni mbali mbali.
Hili la wachaga nalo ni sehemu ya ya maisha.

Mwanadamu ameumbwa kwa namna ya kuweza kuishi kuyaweza mazingira yake.

Kwa hio wasilaumiwe kwa hilo ni sehemu ya maisha.


Mimi ni mchaga na ni wa asili ya huko kilema. Jambo hilo sisi kama famili hatujalifanya na hatutarajii kufanya kitu kama hicho na hakuna athari zozote zimeweza kutokea.
 
sidhani kama ipo siku hiz......ila hilo sale ni la china sio la wachagga...
 
Back
Top Bottom