Mmeongea sana wachambuzi feki, kila mmoja akionyesha ufundi wa kuongea, kana kwamba Simba na Yanga ni Real Madrid au Barca, michuano ya Afrika imeanza na wababe hao wa bongo wamepoteza kwa namna tofauti. Kupoteza kwao kumesababisha wachambuzi wacharuke na hoja, eti ufupi ni tatizo, cjui mabeki hawajui kujipanga, sijui uwezo wetu kimataifa ni mdogo, ungese mtupu.
Mbona Zamalek na ukubwa wake wote kafia nyumbani kwake? Kwahiyo nao wabovu, wana wachezaji wafupi? Ngojeni jumamosi tukawaonyeshe Raja makaburi ya wenzao.
Kila timu ilipoteza kwa mistake za kawaida ila kilatimu ina fursa ya kusonga hatua ya mbele.
Michezo yote miwili niliona vilabu vyetu vilionesha uwezo wa kushinda.
Marekebisho madogo yakifanyiwa kazi tunatoboa kimataifa