Wachambuzi na waandishi wa habari za michezo wa vituo vya redio acheni unafiki

Wachambuzi na waandishi wa habari za michezo wa vituo vya redio acheni unafiki

Chukwu emeka

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2018
Posts
24,314
Reaction score
38,919
Habari wana sports,

Niendelee moja kwa moja kwenye hoja yangu, tangu Yanga yangu ilipokuwa inasuasua mtu aliyerushiwa maneno ni Kocha mkuu Mwinyi Zahera kwamba hana mbinu sahihi, anawachezesha baadhi ya wachezaji out of position, anashindwa kuiunganisha timu, Mara yupo juu ya Yanga hakuna anayeweza kumwambia kitu kwasababu anaisaidia Yanga kwaPesa zake mfukoni na maneno mengiiiiii ya kejeli.Hao hao waandishi za michezo na kelele zao baada ya Mwingi kwenda rikizo na timu ukiwa pre season, walipiga sana kelele, leo ndiyo wa kwanza kumuarika kwenye redio zao na wao kujifanya kumuonea huruma.

Hayo yote yalisemwa na hawa wanaojiita waandishi na wachambuzi nguli wa soka Tz.Kiwango cha Tanzania kuwa hapa hata hawa nao wanachangia maana wanaongea maneno mengi bila takwimu,nikama wanasiasa tu na baadhi ya waandishi wanatumia mic kishabiki sana.

Nikweli Zahera ameisaidia Yanga na alivumilia katika kipindi kigumu sana, na aliendesha harambee kadhaa ambazo kwa wale tulikuwa tunaenda viwanjani msimu uliopita ulienda na pesa ya kiingilio pale taifa unabeba na hela ya kapu lililokuwa linapita kiwanjani ilikusupport team. Mimi ni mmoja wapo wa mtu aliyekuwa anamkubali sana mwingi, ila Kwasasa niseme ukweli nilikuwa sitamani hata kumuona na kufukuzwa kwake nifuraha kubwa sana

Zahera alipoteza weledi kama mwalimu wa mpira, alikuwa amelewa sifa na kusahau kazi yake iliyomleta nchini.heshima aliyopewa alijiona hakuna wakumwambia kitu klabuni.

Kila baada ya mchezo Mwinyi hakosi sababu, na mara nyingi huwa hatoi sababu za kiufundi anapiga blabla tu, juzi anatoka Egypt anasema yaani "Vijana walipambana sana hadi kocha wa Pyramids alikuwa anashangaa", sasa kocha kapigwa 3-0 anajisifu. Kabla ya mchezo wa Pyramids Kirumba "lazima tupate ushindi nyumbani ili tuwe kwenye nafasi nzuri ya kufuzu", baada ya game " hatukujiandaa kucheza mashindano haya na hatuna wachezaji wa kupambana na Pyramids ". Ana kauli nyingi za utata na za kuonyesha kutokuwa na weledi kabisa, japo na viongozi wa hizi timu zetu za urithi wa na changamoto zao ila kwa Mwinyi walikuwa hawana namna zaidi ya kutimua.

Pamoja na mazuri ulioitendea Yanga ila hakuna budi kusema kwaheri viongozi wamefanya maamuzi sahihi, kama unatudai utalipwa tu,Yanga ipo itaendelea kuwepo na tutaiacha.

Daima mbele, Nyuma mwiko

FB_IMG_1572950858707.jpg
 
Zahera dai hela zakooo, au kama VP gombea uenyekiti wa yanga!
 
Nimefuatilia sana uchambuzi wa Wachafu. Nyie mnawaita wasafi.
Wengi wao ni watu wa 5imba na kazi yao kubwa ni kuinanga Yanga.

Wachafu wamekuwa very smart kumuweka Maulid Kitenge ambaye wanajua ni Yanga kuficha nia yao. Maulid ni mtangazaji sio mchambuzi.

Edo hajawahi kuona zuri la Yanga. Kuna Mwingine ndiyo Kwanza namsikia, Ambaruti.
 
Nilikuwa namkubali saba Zahera,ila hizi match mbili za Mwanza na Egypt amenichefua sana, asante sana kwa mazuri yake yote ya msimu uliopita. Kwa heri Zahera.
Nami pia ilikuwa ivyo,ila kauli zake na namna timu inavyocheza na post match analysis yake ilionyesha hana weledi kabisa
 
Tatizo watanzania wanapenda sana kusikia kila lililojema hata kama lina hila ndani yake.Zahera amezungumzia udhaifu wa Yanga ambao tusipoufanyia kazi tutasubiri ubingwa miaka 10 ijayo
 
Hivi nyie vyura mnajua kuna hatari kubwa mbele yenu? Yaani hatari ya kukutana na simba bila zahera? Hii sio hatari tu ni janga! Kama mlinusurika kula saba kwenye zile mechi mbili basi mikono miwili ipo njiani!! Nyie jifanyeni hamtujui tu!
 
Hilo dogo.
Zahera anawadai yanga hela nyingi sanaa.
mishahara yake walikuwa hawampi.
Ngoja Tuone
Tuwaombee wamalizane salama.
Vinginevyo yanga watapelekwa mahakamani
Hivi nyie vyura mnajua kuna hatari kubwa mbele yenu? Yaani hatari ya kukutana na simba bila zahera? Hii sio hatari tu ni janga! Kama mlinusurika kula saba kwenye zile mechi mbili basi mikono miwili ipo njiani!! Nyie jifanyeni hamtujui tu!
 
Tatizo watanzania wanapenda sana kusikia kila lililojema hata kama lina hila ndani yake.Zahera amezungumzia udhaifu wa Yanga ambao tusipoufanyia kazi tutasubiri ubingwa miaka 10 ijayo
Nijambo lipi hilo alilozungumza? Kazi ya mwalimu ni kifundisha mpira
 
Hilo dogo.
Zahera anawadai yanga hela nyingi sanaa.
mishahara yake walikuwa hawampi.
Ngoja Tuone
Tuwaombee wamalizane salama.
Vinginevyo yanga watapelekwa mahakamani
Yanga ni taasisi atalipwa tu
 
Hivi nyie vyura mnajua kuna hatari kubwa mbele yenu? Yaani hatari ya kukutana na simba bila zahera? Hii sio hatari tu ni janga! Kama mlinusurika kula saba kwenye zile mechi mbili basi mikono miwili ipo njiani!! Nyie jifanyeni hamtujui tu!
Ndiyo umbumbumbu wenyewe unadhani Simba kuifunga Yanga ndiyo maendeleo, mbona Yanga inaongoza kwa kuifunga Simba michezo mingi na magoli mengi ila nyie dhaifu ( in Assad voice) ndiyo kelele kibao?
 
Back
Top Bottom