Wachambuzi wa biashara na uchumi mnazungumziaje huu mwenendo wa kola?

Wachambuzi wa biashara na uchumi mnazungumziaje huu mwenendo wa kola?

Makirita Amani

JF-Expert Member
Joined
Jun 6, 2012
Posts
1,915
Reaction score
3,422
Siku za hivi karibuni nimekuwa nikikutana na matangazo mapya mjini yakitangaza ujio wa kinywaji kipa cha MO COLA. Ujio huu umeambatana na vinywaji vingi vya aina hiyo kutoka kampuni ya METL.

Katika kufuatilia kidogo kuhusiana na ujio huuu nilibahatika kukutana na tweet ya Mohamed Dewji ikisema wamewekeza dola milioni 48 kwenye ujio huu wa vinywaji.

Mo Cola will be in the market in 2 weeks. I urge #Tanzanians to try it! We have invested $48 million.
Hii ilinifanya nifikirie cola nyingine ambazo tumekuwa nazo hapa nchini. Tuna sayona cola, azam cola, coca cola, pepsi cola na nyingine ndogo ndogo za kufungwa kwenye vikopo.

Swala kubwa nalofikiria hapa na ninalotaka kuwashirikisha ni je tuna soko kubwa kiasi hiko la hizi cola? Na je Dewji ameingia kwenye competition ambayo ina worth fedha na energy yake?

Najua atakuwa amefanya market research yake ambayo imemridhisha kufikia maamuzi haya ila hapa nataka tuangalie hili soko la cola kwa jicho jingine.
Karibuni.

Samahani kwenye kichwa cha habari ni UCHUMI NA SIO UCHIMU
 
MO ni risk-taker, sifa ya mjasiliamali wa kweli, kuna uwezekano amegundua kuna market share anayoweza kuipata haraka kwny Cola baada ya market research kama ulivyohisi.....I think soon atakuja na Mo-insuarance pia.
 
muda mwngne anaamini anaweza shinda kwa price kua wengne mia8 na yeye anaweza weka mia 6 au mia 5 mana imefika hatua hatununui kitu kutokana na quality kwa sana,tunaangalia bei then quality is a second option,huku watu wanauza brown bread rand 6.5 produced by pick n pay while makampuni mengine wanauza rand 10,so mwisho wa siku pick n pay anauza sana mikate yake while wengne wanauza ila kwa spidi ya kobe na altho ya rand 10 ni mizuri ila watu wanaprefer rand 6.5 coz of cheapnes
 
Ukitaka kunipata ninywe kinywaji niambie habari ya ladha nzuri ya kinywaji na vipi kitalinda afya yangu.

Habari ya umetumia mamilioni ngapi ku invest hainisaidii sana, kwa sababu unaweza kutumia mamilioni ukatengeneza kinywaji kinachosababisha cancer.
 
MO ni risk-taker, sifa ya mjasiliamali wa kweli, kuna uwezekano amegundua kuna market share anayoweza kuipata haraka kwny Cola baada ya market research kama ulivyohisi.....I think soon atakuja na Mo-insuarance pia.

Mkuu mbona hiyo iko kitambo sana, zaidi ya miaka mitano iliyopita sema ilikuwa kwa Jina jingine la Golden Crescent Assurance Co. Ltd mwaka huu ndio kabadilisha jina na kuiita kabisa MO Assurance Company Limited....
 
Ukitaka kunipata ninywe kinywaji niambie habari ya ladha nzuri ya kinywaji na vipi kitalinda afya yangu.

Habari ya umetumia mamilioni ngapi ku invest hainisaidii sana, kwa sababu unaweza kutumia mamilioni ukatengeneza kinywaji kinachosababisha cancer.

kweli kabisa watuambie quality. wakianza kusema wame-invest kiasi gani coca cola atawashinda kwa investment ya kinywaji chake.

nishajaribu hayo ma-azam cola sirudii tena hata waweke bei tsh 200.
 
Unajua biashara ni ujanja na kutambua fursa alichokitumia MO katika hiyo Cola mpya ni ujanja na kucheza na Brand, Cocacola ni Brand kubwa kuliko zote kwa upande wa vinywaji dunia nzima na imeshakuwa Brand nambari 1 inayouza kuliko zote duniani mara nyingi tu, sasa kitu ambacho Mo katumia ni hauwezi ukagelezea kama Cocacola, kwamba labda na wewe bidhaa yako iitwe Cocacola hapana alichokiona kinaleta wateja ni Cola sio Coca hivyo alichochukua kutoka kule ni neno Cola na baada ya hapo akaangalia soko la nyumba ni hapa ni kipi kilichopo akaona Cola zipo nyingi ( Azam,Sayona, Pepsi n.k) akafikira atafanyaje ili apate wateja akafanya ni ujanja Brand ya kinywaji inaitwa Mo-cola lakini kwa chini kidogo imeandikwa inaradha ya machungwa( jifikirie Cola yenye ladha ya orange) lazima watu watakuwa na hamu ya kuijaribu hiyo cola yenye radha ya machungwa tayari anapata wateja na radha ya kinywaji inaweza kuwa yoyote aidha Cola au Orange,mnunuzi hata akikuta radha mbaya au nzuri atajua ndio kinywaji kipya kiko hivyo hata kama itakuwa na taste sawa na zingine yeye atakuwa na advantage ya bidhaa yake inaradha ya machungwa pia.
 
Ukitaka kunipata ninywe kinywaji niambie habari ya ladha nzuri ya kinywaji na vipi kitalinda afya yangu.

Habari ya umetumia mamilioni ngapi ku invest hainisaidii sana, kwa sababu unaweza kutumia mamilioni ukatengeneza kinywaji kinachosababisha cancer.
Labda ndio watanzania wanachotaka kusikia.
Ni kama kwenye elimu, ukijigamba una Phd hata pumba zitapigiwa makofi!
 
nishajaribu hayo ma-azam cola sirudii tena hata waweke bei tsh 200.

Same here..
Ila cha ajabu ina wapenzi wengi sana.
Na hii yote ni kwa sababu ya kuuzwa bei rahisi.
 
Back
Top Bottom