Wachambuzi wetu wa soka wanafaa sana kwa ajili ya watoto wa darasa la saba

Cashman

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2018
Posts
3,017
Reaction score
5,294
Huwa ninaona wachambuzi wetu wa soka wanachokiongelea mara nyingi sio sayansi ya mpira. Nammiss sana Dr Leakey Abdallah kwa vile simuoni mara kwa mara katika kazi hii aliyoifanya vizuri mno kiasi cha kuwafanya watu wengi wavutiwe na soka.

Wachambuzi wengi vijana wamejaa utoto mwingi sana na ambao unaambukiza hadi wachezaji na kuwaathiri kisaikolojia.Mfano ni jinsi walivyoenzi kutetema kwa mayele.Ilifika wakati mtu anaacha kufunga ijapo yupo kwenye nafasi hiyo ili ampe mayele afunge kisha wateteme.Matokeo yake kila mtu anayajua.

Tangu jana naona wana jadili ujinga mwingine wa staili ya kushangilia ya Ambundo. Yaani ukiangalia vitu vinavyojadiliwa ni utoto mwingi sana. Hata hivyo kwa vile hii dunia imejaa wajinga wengi wanapata supporters katika utoto huo.

Sijaona wakiongelea masuala ya mikataba mibovu ya wachezaji, uendeshaji mbaya wa timu, nidhamu kwa wachezaji na viongozi wa timu na hata viwanja vibovu. Kuna mambo mengi ya kuzungumzia lakini hutayasikia zaidi ya kusikia ujinga mwingi sana.

Tulitarajia takwimu za matokeo ya timu zinapokutana katika uwanja kama Kirumba ili mashabiki wajipange kisaikolojia na matokeo ya mechi za Simba na Yanga kwani kwa uwanja ule takwimu zinaibeba Yanga.

Basi tumeshawasema sana lakini naona ni vigumu kuuondoa upumbavu ni kama ndio unaongezeka.

Natamani apatikane game changer kama marehemu Kashasha ili tutoke kwenye huu ujinga.
 
Kinachokutesa ni Mayele na Ambundo tu au Kuna jingine? Hii nchi ukiwa serious Sana unawahi kufa.
 
Umesema kweli aisee....wachamnuzi wa wasafi fm na clouds kidogo wanajitahidi sana.
 
Umeandika meeeeeengiiiiii..... Kinachoonekana tatizo ni Yanga. Punguza ukolo
 
Wachambuzi ambao angalau utasikia wakijadili issues ni Clauds na Wapo radio FM.

Kwingine huko ni utopolo na ujinga pia na ushabiki maandazi with no facts.
 
Hii nchi hakuna kituo cha radio kilicho serious......... na wanafanya hivyo kutokana na wasikilizaji wao wanataka nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…