Wachezaji 20 Simba SC waondoka nchini kuelekea Alexandria Misri kuifuata Al- Ahly

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Msafara wa klabu ya Simba SC, Mnyama ukiwa na wachezaji 20, benchi la ufundi pamoja na baadhi ya viongozi umeondoka nchini leo Januari 29, 2019 kuelekea nchini Misri tayari kuwakabili klabu ya Al-Ahly kwa mchezo wa hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika.

Taarifa inalezwa kuwa msafara wa Simba SC utapitia Addis Ababa nchini Ethiopia na kisha kuelekea mjini Alexandria nchini Misri ambako mchezo huo utachezwa siku ya Jumamosi Februari 2, 2019.

Katika hatua nyingine klabu ya Simba imemteua Patrick Rweyemamu kuwa meneja huku aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo Abbas Ally akitakiwa kuendelea na majukumu yake ya awali kama mratibu wa timu.

This Is Simba Sports Club NguvuMoja



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…