Wachezaji Leicester City Wawasili Thailand Kumzika Mmiliki wa Klabu

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,743
Reaction score
25,564



Wachezaji wa Leicester City wamewasili nchini Thailand kwa mazishi ya mmiliki wa klabu ambaye alifariki kwenye ajali ya helikopta. Jamie Vardy na nahodha wa klabu Wes Morgan ni baadhi ya wachezaji ambao wamehudhuria mazishi ya Vichai Srivaddhanaprabha kwenye hekalu mjini Bangkok. Mazishi hayo yaliyoanza Jumamosi yataendelea kwa wiki nzima. Helikopta hiyo ilianguka baada ya kupaa kutoka uwanja wa mpira wa klabu hiyo tarehe 27 Oktoba na kumuua Vichai na wengine wanne.





Wachezaji wa Leicester walisafiri kwenda Thailand kwa safari ya saa 12 Jumamosi baada ya kushinda kwa bao 1-0 dhidi ya Cardiff kenye ligi ya Premier, mechi yao ya kwanza tangu Vichai afariki. Meneja Claude Puel amewangoza wachezaji wake kwenye mazishi hayo.


Nusara Suknamai, Kaveporn Punpare, rubani Eric Swaffer na mpenzi wake, Izabela Roza Lechowicz, nao walikufa kwenye ajali hiyo. Mazishi ya Bi Nusara yalifanyika Bangkok Jumamosi.


Bi Nusara 32 mmoja wa wafanyakazi wake Vichai alichukua nafasi wa pili kwenye shindano la urembo la mwaka 2005 la Miss Thailand Universe.

















 
inahuzunisha kweli, pole sana kwa walioguswa na wapenzi wa soka kiujumla
 
Aisee acha ule ukanda una madon wa kutisha sana humjui Thaksin Shinawatra
 
"
Bi Nusara 32 mmoja wa wafanyakazi wake Vichai alichukua nafasi wa pili kwenye shindano la urembo la mwaka 2005 la Miss Thailand Universe."

Huyu Miss alikuwa mfanyakazi wake kweli ? Basi sawa

R.I.P
UKIFIKA NAWEWE UKO UWAULIZE
 
R I P Vichai
Your surname /family name is cumbersome to me.
See you in glory!
 
Kwa wajuzi wa kithailand mtusaidie hili jina jinsi linavyotamkwa:- "Srivaddhanaprabhar"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…