Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 2,428
- 3,937
Nimewaza ni nafasi gani hii adimu sana ambayo wachezaji wa Taifa Stars wamepata ya kuonekana kuonyesha vipaji vyao. Nikasema kweli Mungu hamtupi mja wake!
Platform kubwa kama hii wachezaji wa michezo mbalimbali wanaojitambua walipoipata waliitumia ipasavyo kuonyesha mambo mbalimbali ambayo labda taifa au dunia haiyapi kipaumbele inavyostahili. Kuna mambo ya unyanyasaji wa kijinsia, uhuru wa kujieleza, ukandamizaji na uonevu unaofanywa na wenye mamlaka na nguvu, haki za binadamu, nk.
Nikawakumbuka wachezaji mbalimbali duniani, tena wakubwa tu na wenye vipaji vya hali ya juu ambao walikuwa na vingi vya kupoteza (mali, mikataba minono, kazi zao, mashabiki, nk.). Hao walitumia nafasi hizo kufanya maamuzi haya na mpaka leo na labda hata milele, dunia itaheshimu kujitoa kwao kwa ajili ya wengine.
Kufanya mambo haya inahitaji kuweka ubinafsi pembeni na kuangalia mahitaji ya wengi na pia vizazi vijavyo. Hawa watu hawakurubuniwa kwa mikataba minono au ahadi za viwanja kule Washington DC au New York.
Kuna hadi walioenda jela kama Muhammad Ali, lakini leo hii ukitaja wanamichezo waliowahi kuheshimika duniani hawezi kukosa.
Nawakumbusha tu historia inavyoandikwaga.
Platform kubwa kama hii wachezaji wa michezo mbalimbali wanaojitambua walipoipata waliitumia ipasavyo kuonyesha mambo mbalimbali ambayo labda taifa au dunia haiyapi kipaumbele inavyostahili. Kuna mambo ya unyanyasaji wa kijinsia, uhuru wa kujieleza, ukandamizaji na uonevu unaofanywa na wenye mamlaka na nguvu, haki za binadamu, nk.
Nikawakumbuka wachezaji mbalimbali duniani, tena wakubwa tu na wenye vipaji vya hali ya juu ambao walikuwa na vingi vya kupoteza (mali, mikataba minono, kazi zao, mashabiki, nk.). Hao walitumia nafasi hizo kufanya maamuzi haya na mpaka leo na labda hata milele, dunia itaheshimu kujitoa kwao kwa ajili ya wengine.
Kufanya mambo haya inahitaji kuweka ubinafsi pembeni na kuangalia mahitaji ya wengi na pia vizazi vijavyo. Hawa watu hawakurubuniwa kwa mikataba minono au ahadi za viwanja kule Washington DC au New York.
Kuna hadi walioenda jela kama Muhammad Ali, lakini leo hii ukitaja wanamichezo waliowahi kuheshimika duniani hawezi kukosa.
Nawakumbusha tu historia inavyoandikwaga.