wachezaji wa wenzetu

Unataka kuzungumzia urefu au maelekezo ya kocha na mchezaji?!!:confused2:
 
Hawa waganda ni noma bwana lazima tukiri, nimeangalia hio mechi na huyu jamaa ndie aliyefunga goli la kwanza, real wako safi kwa stamina na skills, hebu tucompare na wetu juzi walipokuwa wanacheza na algeria, daaa sijui wanakula hewa au nini maana wakipigwa kapush kidogo tu wanadondoka.Wajitahidi kujenga miili yao kwa chakula cha kutia nguvu sio kula chipsi tu, mazoezi magumuuu halafu kula kidogo lazima wachezaji wakomae.
 
Kuna Kocha Moja Tanzania alisha shauri tuwe na wachezaji wenye nguvu, kama zamani akina Makumbi Juma, Juma Mkambi, Abdallah Buruhani, Mohamed Tall nk, na pia tuji linganishe na wachezaji wa timu za wenzetu, kama Senegal, Nigeria, Cameroon, Zimbabwe nk,
 

Linawezekana iwapo tutawafuata huko waliko na kuwafundisha kucheza soka. Kwa sasa wapo wanaendelea na kilimo na wanajitayarisha na msimu ujao wa kilimo.
Kwao kila jioni hujikusanya kwenye vilabu vya pombe za kienyeji wakipiga soga,weekend ukienda katika viwanja vya shule za msingi utashangaa kuona vipaji vya soka lakini vimekosa maarifa ya kiuchezaji.
Wana stamina ya hali ya juu,wana pumzi ya kutosha,wana mbio na mashuti makali.Tukiamini kuwa mchezaji mzuri lazima afike Dar (japo si vibaya maana ndipo kwenye Coverage kubwa)hatutawafikia,watabaki hukohuko wakisikilza redioni na kushangilia maana nao wanazipenda timu hizi na wengine siku hizi wana solar na madish majumbani mwao hivyo huwa wanapata nafasi ya kumuangalia Rooney,Drogba,Defoe n.k.
Hebu ikumbuke Tukuyu Stars,ilijaza Giants watupu ule msimu wake wa kwanza na wa pili.....
Tuache uvivu tukasake vipaji remote areas kwa. vile hatuwezi kurudisha UMISETA kama ya enzi zile
 

Duh wengine wanauza vyuma chakavu na wengine ni teksi drivers.! ndiko wanakoishia wachezaji wetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…