Wachina kujenga Bandari ya Bagamoyo ni ndoto au kuna uhalisia?

Wachina kujenga Bandari ya Bagamoyo ni ndoto au kuna uhalisia?

Hute

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,537
Reaction score
6,472
Hebu naomba kuuliza kwa wale walio jikoni kama wamo humu JF, hivi kweli hili suala la Wachina kujenga bandari kubwa bagamoyo, ni kitu cha kweli au ni ahadi za hewani tu? Nimeuliza hivi kwasababu Julius Nyerere Airport waliahidi kuwa watajenga airport, wakachora mchoro mzuri wa tanzanite, wakazungusha hadi ukuta wa mabanzi, matokeo yake naona hata mabanzi wameyatoa na mchoro umebadilika.

Walikikosa kitu gani pale Julius Nyerere wakaamua kuachana na Tanzania wasiendelee kujenga? Pili, hicho kilichowafanya waiache airport hakiwezi kuwafanya waachane na bandari hiyo wanayotutia moyo?

Mimi sitaamini kama kutakuwa na Bandari hadi nione imeshaanza kujengwa, kwa maneno tu hivi najua tunapigwa changa la macho. Kama ni kweli wanaanza kujenga ni lini? Kuna dalili zozote kwa wale walioko serikalini na wale wa Bagamoyo kuwa wameshaanza au wataanza hivi karibuni?

Pili, kitu gani kinatushinda Watanzania kuboresha reli ya TAZARA na reli ya Kati? Kama wamiliki wa malori ndio kikwazo, kweli wametushinda? Kitu gani pia kitatushinda kuunganisha reli ya kati na reli ya TAZARA kuanza kuwa na treni za umeme? Ili mimi nisafiri toka Kigoma hadi Dar es Salaam kwa masaa walau kumi au kumi na mbili kuliko kutembea siku moja, ili container likipakiwa Dar es Salaam lifike siku hiyohiyo mpakani na Burundi na Congo.

Kitu gani kinatushinda Watanzania kubadilisha reli ya TAZARA kutumia umeme kuliko mafuta, si Muhongo anasema 2015 tutakuwa na umeme wa kuuza hadi nje? Sasa, kama umeme tutakuwa nao bwerere, kitu gani kitatushinda sisi kuwa na treni za mwendo kasi na zinazotumia umeme?

Kama vipi hao wamiliki wa malori wanaokwambisha treni waundikwe kikosi kazi maalumu cha kuwadhibiti kwani hao ni wahujumu uchumi na maadui wa maendeleo ya Tanzania. Tanzania tutalala hadi lini jamani? Rasilimali tunazo, tunashindwa kuzitumia kweli?
 
mimi nisipoiona imeanza kujengwa, sitakuja kuamini. basi jk awaambie wachina wachangamke kuanza maandalizi ya kujenga kama kweli icho kitu kipo. nafikiri jk anatakiwa kufanya reprisal kwa yale yanayofanywa na kenya uganda na rwanda, ajue kuwa sasaivi Tanzania ipo kwenye vita vya kiuchumi si vita vya mtutu bali vita vya kiuchumi kati yake na kenya. wakenya wamepaniki baada ya kuona dalili za mafanikio tz, kwa kuona gas, madini, marais wakubwa kuja na kusaini mikataba minono, bandari kubwa kuliko zote africa etc, hivyo wanaogopa ile dhana kwamba kenya is the biggest economy in east africa inaenda kuchukuliwa na tz, hivyo wanapigana vita vya kiuchumi vya chini kwa chini, jk awaambie wachina waanza kujenga bandari, tuchangamke watz ili tuipiku kenya.
 
mimi nisipoiona imeanza kujengwa, sitakuja kuamini. basi jk awaambie wachina wachangamke kuanza maandalizi ya kujenga kama kweli icho kitu kipo. nafikiri jk anatakiwa kufanya reprisal kwa yale yanayofanywa na kenya uganda na rwanda, ajue kuwa sasaivi Tanzania ipo kwenye vita vya kiuchumi si vita vya mtutu bali vita vya kiuchumi kati yake na kenya. wakenya wamepaniki baada ya kuona dalili za mafanikio tz, kwa kuona gas, madini, marais wakubwa kuja na kusaini mikataba minono, bandari kubwa kuliko zote africa etc, hivyo wanaogopa ile dhana kwamba kenya is the biggest economy in east africa inaenda kuchukuliwa na tz, hivyo wanapigana vita vya kiuchumi vya chini kwa chini, jk awaambie wachina waanza kujenga bandari, tuchangamke watz ili tuipiku kenya.

Ndugu Hute, unaweza kuwa TOMASO hadi uone lakini hiyo miradi ni kweli ipo na inatekelzwa. Kinyume na utaratibu wa zamani serikali kufanya kila kitu wenyewe, sasa hivi uwekezaji unaenda kwa mtindo wa PPP (Public Private Partnership) na private sector wanasukumwa zaidi na faida.

Jaribu kupitia mabandiko kadhaa katika ukurasa huu utapa taarifa zote muhimu juu ya miradi hii, hapa JF ni zaidi ya Google.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu Hute, unaweza kuwa TOMASO hadi uone lakini hiyo miradi ni kweli ipo na inatekelzwa. Kinyume na utaratibu wa zamani serikali kufanya kila kitu wenyewe, sasa hivi uwekezaji unaenda kwa mtindo wa PPP (Public Private Partnership) na private sector wanasukumwa zaidi na faida.

Jaribu kupitia mabandiko kadhaa katika ukurasa huu utapa taarifa zote muhimu juu ya miradi hii, hapa JF ni zaidi ya Google.
hiyo public private partnership ilifanyaje uwanja wa jk nyerere, mbona umepigwa chini? tena na wachina haohao...tutawaaminije kama hawawezi kurukia kenya? sina imani nao
 
hebu naomba kuuliza kwa wale walio jikoni kama wamo humu jf. hivi kweli hili suala la wachina kujenga bandari kuuuuubwa bagamoyo, ni kitu cha kweli au ni ahadi za hewani tu? nimeuliza hivi kwasababu JK NYERERE AIRPORT waliahidi kuwa watajenga airport, wakachora mchoro mzuriiii wa tanzanite,wakazungusha hadi ukuta wa mabanzi, matokeo yake naona hata mabanzi wameyatoa na mchoro umebadilika. walikikosa kitu gani pale jk nyerere wakaamua kuachana na tz wasiendelee kujenga?, pili, hicho kilichowafanya waiache airport hakiwezi kuwafanya waachane na bandari hiyo wanayotutia moyo? MIMI SITAAMINI KAMA KUTAKUWA NA BANDARI HADI NIONE IMESHAANZA KUJENGWA, kwa maneno tuhivi najua tunapigwa changa la macho. kama ni kweli wanaanza kujenga lini, kuna dalili zozote kwa wale walioko serikalini na wale wa bagamoyo kuwa wameshaanza au wataanza hivi karibuni?

pili, kitu gani kinatushinda watz kuboresha reli ya TAZARA na reli ya KATI? kama wamiliki wa malori ndio kikwazo, kweli wametushinda? kitu gani pia kitatushinda kuunganisha reli ya kati na reli ya tazara kuanza kuwa na treni za umeme? ili mimi nisafiri toka kigoma hadi dsm kwa masaa walau kumi au kumi na mbili kuliko kutembea siku moja, ili container likipakiwa dsm lifike siku hiyohiyo mpakani na burundi na congo,

kitu gani kinatushinda watz kubadilisha reli ya tazara kutumia umeme kuliko mafuta, si muhongo anasema 2015 tutakuwa na umeme wa kuuza hadi nje? sasa, kama umeme tutakuwa nao bwerere, kitu gani kitatushinda sisi kuwa na treni za mwendo kasi na zinazotumia umeme? kama vipi hao wamiliki wa malori wanaokwambisha treni waundikwe kikosi kazi maalumu cha kuwadhibiti kwani hao ni wahujumu uchumi na maadui wa maendeleo ya tz. Tanzania tutalala hadi lini jamani? rasilimali tunazo, tunashindwa kuzitumia kweli?


Toa chuki moyoni ndugu yangu... Rasili mali ya kweli ni moyo mkunjufu. Sio roho korosho kama yako.
 
wachina waongo tu. walisema 2017 itakuwa imeshaisha, hadi sasaivi hawajasembua hata hatua moja. changa la macho t u.
 
Back
Top Bottom