Emc2
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 16,808
- 16,887
Dar es Salaam. China inakusudia kujenga Kituo cha Kisasa cha Kibiashara katika eneo la Ubungo, kikiwa na uwezo wa kukusanya shughuli zote za biashara na mahitaji ya nyumbani.
Kituo ambacho kitakapokamilika kitalifanya Jiji la Dar es Salaam lifahamike kama ‘Dubai ndogo ya Tanzania’.
Pia, kituo hicho ambacho ujenzi wake unatarajiwa kuanza mwaka huu na kukamilika baada ya miezi 15, kinatajwa kuwa tofauti na Soko Kuu la Kariakoo, kitakuwa na zaidi ya maduka 3,000, maghala madogo zaidi 300 na eneo lenye uwezo wa kuhifadhi magari 5,000. Kitajengwa na Kampuni ya LingHang na kusimamiwa na Serikali ya China.
Wachina kujenga Dubai ndogo ya Tanzania Ubungo
http://www.skyscrapercity.com/showthread.php?p=142674363#post142674363