Wachungaji wa kibongo wanazingua

Wachungaji wa kibongo wanazingua

msukule mzembe

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2022
Posts
253
Reaction score
302
Juzi jumapili nikasema ngoja niende kanisani kwanza japo nikashiriki na watu katika ibada ya hapa na pale nikachukua kagari kangu ka ist kabovu nikatoka magetoni kipati mbagala hadi keko kanisa la universal.

Ile kutimba ndani kanisanu muhuni sina hili wala lile nikatafuta siti nzuri ya mbele ili nikakae, nikaona pembeni kuna pisi moja imetulia nikaona sio mbaya nikienda kukaa karibu nayo angalau tubadilishane hata chaji mbili tatu, nikaifata nikaisalimia kwa jina la bwana nae akaitikia nikamwambia nampenda nae mlokole yule akajibu ananipenda pia kwa jina la yesu, nikaona leo kitaumana.

Muda wa mchungaji kuja kuhubiri ulipofika nikashangaa kila alipokua akihubiri akiongelea dhambi ya aina yoyote ile ananiangalia mimi na kidole anakionesha kwangu kimtindo mtindo, nikavumilia ila baada ya muda had watu wakaanza kusanuka wakawa wananiangalia, akisema uzinzi basi ataniangalia mimi, ulevi, uasherati na dhambi zote kwangu........................[emoji41][emoji41][emoji41]

Kiufupi wachungaji habari hizo muache, mnatuharibia sana waumini wenu mnatuchoresha kimtindo

Nawasilisha madini[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
nikaona pembeni kuna pisi moja imetulia nikaona sio mbaya nikienda kukaa karibu nayo angalau tubadilishane hata chaji mbili tatu, nikaifata nikaisalimia kwa jina la bwana nae akaitikia nikamwambia nampenda nae mlokole yule akajibu ananipenda pia kwa jina la yesu,
nikaona leo
😂😂Mwisho wa ibada kiliumana, au?!


muda wa mchungaji kuja kuhubiri ulupofika nikashangaa kila alipokua akihubiri akiongelea dhambi ya aina yoyote ile ananiangalia mimi na kidole anakionesha kwangu kimtindo mtindo, nikavumilia ila baada ya muda had watu wakaanza kusanuka wakawa wananiangalia, akisema uzinzi basi ataniangalia mimi, ulevi , uasherati na dhambi zote kwangu........................
emoji41.png
emoji41.png
emoji41.png
😂😂😅 Aisee!
 
Pengine huyo mchungaji kila siku hua anaonyesha kidole upande huo huo,sasa kwavile wewe ni mgeni ukajua anakupoint wewe.

Watu walianza kukuangalia wewe coz ulijishtukia na hukua comfortable.

Ila hii ni kama Chai vile sema imepoa tu.
 
Mchungaji angemezea, ajue mwanamke ni sawa na kiti cha daladala, ukiona mtu kakaa seat unayoipenda tafuta nyingine.
 
Ilikuwa pisi ya mchungaji hiyo maana aliona ishara fulani za kupigiwa.
 
Hii stori naona ipo nusu nusu kwanza tuambie ulishia wapi na pis .....pili hiyo piss inaonekana ni ya pasta we umeleta shobo ... au ndo kimasihara mkuu
 
Ungehamia siti nyengine je angeendelea kukunyoshea kidole?
 
Back
Top Bottom