TANGAZO
BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
Baraza la Mitihani la Tanzania linapenda kuwakumbusha watu wote wanaotaka kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne
(CSEE) na Maarifa
(QT) mwezi
Novemba, 2014 kama Watahiniwa wa Kujitegemea kwamba kipindi cha usajili kilichoanza rasmi tarehe
1 Januari, 2014 kwa ada ya Shilingi
50,000/=kwa wanaojisajili
CSEE na Shilingi
30,000/= kwa wanaojisajili
QT kitaishia tarehe
28 Februari, 2014.
Waombaji wote
wanasisitizwa kuhakikisha wanajisajili mapema kwa njia ya mtandao kupitia tovuti ya Baraza la Mitihani ya
www.necta.go.tz. Kabla ya kujisajili kwenye mtandao, waombaji wanapaswa kwenda kwenye vituo vya mitihani kuchukua namba rejea (reference number) zinazotolewa
bure na kulipa ada ya mtihani kwa njia ya Posta au Mpesa.
Imetolewa na:
KAIMU KATIBU MTENDAJI
BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA.