Wadau naomba msaada kwa wanaofahamu taratibu!

Wadau naomba msaada kwa wanaofahamu taratibu!

kikaniki

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2014
Posts
508
Reaction score
968
Mwaka juzi nililima mahindi kijijini (mimi nakaa mjini, nimeajiriwa).

Kule kijijini, kuna mama mmoja alikuwa ananisaidia kulisimamia shamba hilo kuanzia kulimwa, kupanda hadi mavuno). Na alifanya hivyo bila mimi kuwepo (kulima kwa simu)[emoji3]. Mimi kazi yangu ilikuwa ni kutuma pesa tu.

Alipovuna, aliniambia kuwa nimepata magunia 150 ya mahindi. Nikamshukuru snaa na nikamwambia, achukue magunia 20 na mimi aniachie magunia 130.

Sasa kuna kipindi nikawa na shida ya pesa. Nikamwambia ayauze mahindi yangu na anitumie pesa. Huu ni mwaka wa pili sasa ananisumbua. Ananiambia anatuma na hatumi. Nawaza kumfuata kijijini, ila nahofia tunaweza kuumizana na mambo yakawa ndivyo sivyo.

Sasa nataka kumfungulia mashtaka. Nataka kumfungulia kesi ya madai.

Taratibu za ufunguaji wa kesi za madai ni upi?

NB:-
Nina ushahidi wa meseji ambazo tumekuwa tunawasiliana nae tangu hatua za mwanzo kabisa hadi sasa.

Nina ushahidi wa meseji za kutuma pesa kwake na meseji za kunijibu kuwa kapokea

Nina ushahidi wa mawasiliano yangu na mtoto/kijana wake ambaye ndiye anafahamu mapatano kati yangu na mama yake.

Nina ushahidi wa sauti/sound clips ambazo nimekuwa nikimrekodi kila nikiongea nae.

Naombeni taratibu za kufuata ili nimfungulie kesi..pia naomba kujua gharama za kufungua kesi ya madai

Na je, naweza kumfungulia kesi ya madai na ya jinai katika kipindi kimoja?
 
Mwaka juzi nililima mahindi kijijini (mimi nakaa mjini, nimeajiriwa).

Kule kijijini, kuna mama mmoja alikuwa ananisaidia kulisimamia shamba hilo kuanzia kulimwa, kupanda hadi mavuno). Na alifanya hivyo bila mimi kuwepo (kulima kwa simu)[emoji3]. Mimi kazi yangu ilikuwa ni kutuma pesa tu.

Alipovuna, aliniambia kuwa nimepata magunia 150 ya mahindi. Nikamshukuru snaa na nikamwambia, achukue magunia 20 na mimi aniachie magunia 130.

Sasa kuna kipindi nikawa na shida ya pesa. Nikamwambia ayauze mahindi yangu na anitumie pesa. Huu ni mwaka wa pili sasa ananisumbua. Ananiambia anatuma na hatumi. Nawaza kumfuata kijijini, ila nahofia tunaweza kuumizana na mambo yakawa ndivyo sivyo.

Sasa nataka kumfungulia mashtaka. Nataka kumfungulia kesi ya madai.

Taratibu za ufunguaji wa kesi za madai ni upi?

NB:-
Nina ushahidi wa meseji ambazo tumekuwa tunawasiliana nae tangu hatua za mwanzo kabisa hadi sasa.

Nina ushahidi wa meseji za kutuma pesa kwake na meseji za kunijibu kuwa kapokea

Nina ushahidi wa mawasiliano yangu na mtoto/kijana wake ambaye ndiye anafahamu mapatano kati yangu na mama yake.

Nina ushahidi wa sauti/sound clips ambazo nimekuwa nikimrekodi kila nikiongea nae.

Naombeni taratibu za kufuata ili nimfungulie kesi..pia naomba kujua gharama za kufungua kesi ya madai

Na je, naweza kumfungulia kesi ya madai na ya jinai katika kipindi kimoja?
Jaribu kuwa serious wakati mwingne
 
Jamaa yaani umewekeza hela na hata kwenda kufuatilia kwa karibu hukwenda kana kwamba ulilima Somalia?

Sasa kama ulikuwa bize kwenye kwenda shambani, utaweza danadana za mahakamani?.

Hebu kuwa siriazi kidogo jamaa 😅😅😅😅😅

Acha upigwe tu! Na huyo maza humuwezi
 
Uyo hajitambui na mahakamani atakutana na mawakili wajanja wampige tena
Jamaa yaani umewekeza hela na hata kwenda kufuatilia kwa karibu hukwenda kana kwamba ulilima Somalia?

Sasa kama ulikuwa bize kwenye kwenda shambani, utaweza danadana za mahakamani?.

Hebu kuwa siriazi kidogo jamaa [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]

Acha upigwe tu! Na huyo maza humuwezi
 
We jamaa ban, ss km huwezi kufatilia jambo kwanini uamue kulifanya. Hata km mm ndo ningekua uyo bibi ningekula ela yako
 
Umepigwa.
Unatuma hela eti gunia 150, ulishindwa hata weekend moja kuchomoka fasta ?

Jaribu tena wakati mwingine
 
Swali linasema
Assume gravitational force constant is 5N/M^2 . Mtu anasema g haiwezi kuwa hiyo,ni 9.8.


Mtakiwa kutoa ushauri kutokana na tatizo lililotokea,mnashindwa vipi kuwa flexible?
 
Mwaka juzi nililima mahindi kijijini (mimi nakaa mjini, nimeajiriwa).

Kule kijijini, kuna mama mmoja alikuwa ananisaidia kulisimamia shamba hilo kuanzia kulimwa, kupanda hadi mavuno). Na alifanya hivyo bila mimi kuwepo (kulima kwa simu)[emoji3]. Mimi kazi yangu ilikuwa ni kutuma pesa tu.

Alipovuna, aliniambia kuwa nimepata magunia 150 ya mahindi. Nikamshukuru snaa na nikamwambia, achukue magunia 20 na mimi aniachie magunia 130.

Sasa kuna kipindi nikawa na shida ya pesa. Nikamwambia ayauze mahindi yangu na anitumie pesa. Huu ni mwaka wa pili sasa ananisumbua. Ananiambia anatuma na hatumi. Nawaza kumfuata kijijini, ila nahofia tunaweza kuumizana na mambo yakawa ndivyo sivyo.

Sasa nataka kumfungulia mashtaka. Nataka kumfungulia kesi ya madai.

Taratibu za ufunguaji wa kesi za madai ni upi?

NB:-
Nina ushahidi wa meseji ambazo tumekuwa tunawasiliana nae tangu hatua za mwanzo kabisa hadi sasa.

Nina ushahidi wa meseji za kutuma pesa kwake na meseji za kunijibu kuwa kapokea

Nina ushahidi wa mawasiliano yangu na mtoto/kijana wake ambaye ndiye anafahamu mapatano kati yangu na mama yake.

Nina ushahidi wa sauti/sound clips ambazo nimekuwa nikimrekodi kila nikiongea nae.

Naombeni taratibu za kufuata ili nimfungulie kesi..pia naomba kujua gharama za kufungua kesi ya madai

Na je, naweza kumfungulia kesi ya madai na ya jinai katika kipindi kimoja?
1. Ainisha kwa mchanganuo, kiasi cha fedha unachomdai huyo bibi

2. Andika hati ya madai na umpe huyo bibi kuwa akilipe fedha yako kwa muda flani (wiki 2, mwezi nk)

3. Kiwango cha fedha unachodai ni cha muhimu sana kujulikana kwa maana ndicho kitachokueleza mahakama unayoswa kwenda
 
duh,kama unafanya biashara ambayo hata siku moja hujawahi kufika kuiona wala kukagua bora uendelee kubana mshahara wako ni ushauri tu

Sent from my CAM-AL00 using JamiiForums mobile app
 
duh,kama unafanya biashara ambayo hata siku moja hujawahi kufika kuiona wala kukagua bora uendelee kubana mshahara wako ni ushauri tu

Sent from my CAM-AL00 using JamiiForums mobile app
Usikariri sana! Siyo kila biashara lazima uwepo wwe mwenyewe! Umesha kabizi majukumu wwe Ni kuwasiliana ki mtandao tu maana hata bank siyo lazima ukatowe au kuweka unaweza fanya transfer zako kimtandao tu na siyo lazima eti uwendee Bank ukaangalie pesa Zako zinaendeleaje!!!??
 
Ukienda mahakamani watapokea malalamiko yako, lakini hiyo kesi itakaa inapigwa kalenda miaka nenda rudi, fanya mambo mengine.
 
Back
Top Bottom