Wadau naombeni ushauri jinsi ya kuwekeza hizi shs. 10,000,000

Mkuu umeshakosea hatua ya kwanza kwa kukopa bila kuwa na wazo la uhakika, angalia hizo pesa zisije kuishia kwenye matatizo ya nyumbani ushauri ninao weza kukupa kwa sasa hivi kama hilo wazo la spea za magari unaliamini na ndio mkombozi wako tafuta wataalamu wa kutengeneza mipango biashara waeleze wakufanyie mchanganuo na huo mpango biashara wako ndio uanze hiyo biashara, hauwezi ukawa na wazo bila eneo mkuu sababu wazo hupatikana kwenye eneo husika mfano mtaani kuna magari mengi na garage lakini hakuna duka linalouza spea za hayo magari tayari umepata wazo na eneo la kuliweka wazo hilo nimeshangaa kidogo kwa wazo lako isije ikawa ni la kushauriwa na marafiki au kwa vile fulani anafanya
 
Hongera kwa kufikiria kufanya biashara lakini kwa sasa huna tofauti sana na hao wenzio waliokopa na kununua magari. Walionunua viwanja hawajapotea sana labda kama wamenunua bonde la mpunga. Wakifulia wanaweza kuviuza au kuvitumia kama rehani kukopa. Mpaka sasa nadhani aliyekukopesha keshaanza kukata hela yake na riba wakati hela uliyochukua imekaa tu ikizidi kushuka thamani kama magari ya wale wafanyakazi wengine.

Kuhusu hiyo biashara unayotaka kufanya wengi wameshasema mengi na kuhoji maswali ya msingi sana. Mi nachojua hakuna kanuni maalum ya kuanza biashara ila kuna mambo ya msingi yasipozingatiwa biashara inakufa. Mi nilipata wazo la kufanya biashara baada ya kuona msingi wa fremu unachimbwa. Kwa kutambua uzuri wa eneo lile kwa maana ya idadi ya watu (wateja watarajiwa) nikaenda kuwahi fremu bila kujua nitafanya biashara gani. Baada ya kulipia hela ya kushika fremu ndo nikaanza kufikiri cha kufanya. Nilipopata wazo nikaenda kukopa. Mwaka wa kwanza na wa pili biashara ilikuwa tamu mno. Hela niliyokopa ilirudi ndani ya mwaka wa kwanza. Mwaka wa pili waswahili kama kawaida wakaona nafaidi wakaanza kufanya biashara kama yangu. Akaanza wa kwanza, wa pili...mi nikaendelea tu bila kuchukua tahadhari yoyote ya kukabiliana na ule ushindani. Baadae wakafika kama 6 hivi. Tukajikuta kila mtu anapata wateja "wawili wawili", maisha ya kibiashara yakaanza kuwa magumu, nikafikia mahali pa kuhudumia biashara kwa hela ya mshahara. Mwishowe nikaamua kuifungia mbali na hela za mtaji nikazipeleka benki ili nijipange upya. Loh!

Kwa tahadhari tu fanya kama walivyokushauri wale waliosema hiyo hela weka kwenye akaunti yenye riba mpaka utakapokuwa tayari, au baada ya kuwaona washauri wa biashara wekeza kwenye biashara ambayo imeshaanza we uwe unakula faida japo itakuwa ndogo (mi naitaka hii na nitaomba mawazo zaidi) kwani mojawapo ya mambo niliyojifunza kama mfanyabiashara ambaye ni mwajiriwa na sijataka kuachia ajira ni ugumu wa kuwatumikia mabwana wawili. Biashara nyingi zinahitaji usimamizi wa karibu sana hasa mwanzoni; utaweza kujigawa au utakuwa kama walimu wa shule kama benjamin mkapa wanapiga hata miezi miwili hawajakanyaga darasani? Kuna mwenzangu alikopa m 10 akafungua biashara nzuri sana lakini ilimlipa miezi kama 5 wafanyakazi wakamzidi ujanja, ikafa kifo cha mende. Alipouza kilichokuwa kimebaki aliambulia m 2 tu.

Mwingine aliyekopa kama wewe kabla ya kujua anachotaka kufanya, alijikuta ameanza kuchomoa hapo kidogo kidogo. Alichofanya ni kuzibadilisha zikawa dola ili kuepuka vishawishi vya kuzivuta kwa simu toka akaunti ya akiba ya madafu, lakini pia sijui uchumi ila nadhani zikiwa dola ni salama kuliko madafu kwa maana ya ile hatari ya kushuka thamani.

Kila la heri.
 

Mkuu umetoa ushauri mzuri sana. Halafu mimi pia nina biashara ambayo nahitaji mtu awekeze mtaji tu awe akila faida kila mwezi. Kama unahitaji tuwasiliane zaidi.
 

Asante sana kwa ufafanuzi mzuri, ngoja nijipange kwa ajili ya kilimo hicho. Halafu nitahitaji usaidizi wako katika kilimo pamoja na kupata vibarua wa kilimo na palizi na ikiwezekana msimamizi mwaminifu kama atahitajika maana mimi nitakuwa nakuja siku za week end na sikukuu. Je inawezekana? Haiwezi kuniletea matatizo?
 
Kimbiji si Kigamboni, ni maeneo tofauti kabisa.Kuuza, kununuua na kuendeleza ni hiari yako , mali ni yako Tanzania si ya miaka ile ambayo watu wananyimwa haki zao au kudhurumiwa kirahisi.Usiwe na mawazo mgando!
 
Kweli watu wanaweza kukufanya ukaogopa na hta ukashindwa kujaribu yani chini ya mil 100 hufanyi biashara hio hilo siamini mpaka kesho kwa ushauri tu weka mil 5 pemben kisha wekeza 5 kwanza halafu sio lazma frem iwe kwenye maeneo ghali we chakufanya tafuta jirani na kituo cha waendesha bodaboda na umpate fundi wa kuwa anakaa barazani kwako au jirani ili yeye ndo atakuletea watu
nina mfano hai kabisa kama unaweza fika tabata segerea kituo cha chama pale uone mwenyewe jamaa anauza spare za boda boda na matengenezo hapo hapo
Usiogope mkuu Mungu atakua nawe sina shaka utafanikiwa nasubiri kwa hamu kusikia ushuhuda wako jf
Success does not come easily na failure is not loosing but a lesson worthy to learn
GOOD LUCK
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…