Njoo kama kwingine kote umekosa ndugu. Uwe tayari kwa yafuatayo:
1.Utaitwa jina la mahudhurio darasani kama darasa la kwanza yaani ile "present sir/madam" kama mahudhurio kwa semester ni below 85% utarudia darasa.
2.Utafelishwa makusudi kama chuo kinahitaji fedha kwa muda huo kwani supp. 1=10000. Wakitengeneza supp 500 kwa semester shughuli zao zinaenda sawa.
3. Utauziwa madaftari yenye nembo ya Chuo kwa sh 100000 kwa mwaka (lazima)
4.Hutapewa special pepa kama umepata udhuru wa aina yoyote(umefiwa, unaumwa, umejifungua(ke) n.k). Utarudia mwaka.
5. Kuhitimu na kupewa cheti ni vitu viwili tofauti. Ukimaliza masomo nenda kwenu, cheti utaitwa kuchukua wakijiskia wenyewe hata baada ya 2yrs.
6.Ukikorofishana na muhindi yeyote au utawala wa chuo, adhabu ni moja tu. Hufukuzwi. Utapewa Sup. Utaifanya,utafeli tena. Utarudia mwaka. Utarudia tena na tena. Kuna watu wana miaka 7 toka waanze.
Karibu