Nyange
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 3,517
- 1,869
Habari za leo wakuu, jana nilihojiana na baadhi ya wana jamii wenzangu ili kubaini kwannn watu wenye sifa za kupiga kura lakn hawapigi kura. Wametoa sababu zifuatazo:-
TUWASHAURI JE HAWA WATU? Na wasilisha.
- Mmoja amedai NEC inalipa wafanyakazi mishahara mikubwa, imeajili wataala wa fani mbalimbali, zikiwemo IT, la ajabu ni kwamba mpaka sasa hawajatoa list za wapiga kura ili kila mtu ajitambue yuko list No gain ili kwake iwe rahisi cku ya uchaguzi ajipange kwenye msari sahihi, ili asipoteze muda. Wanadai hii ni hujuma No 1. ana uliza kwaninn majina yasitolewe mapema watu wajiandae kila m2 kwa wakati wake aende kpiga kura?
- Mwingine amedai kuwa kwenye maeneo yanayo dhaniwa kuwa thithiem haipati kura, hawapeleki vifaa vya kutosha nap engine wanapeleka kiduchu ili watu wakate tama wahairishe kupiga kura.
- Mwingine alidai TZ hakuna demokrasia, make hata maeneo yanayo dhaniwa wapinzani wana nguvu, matokeo huchukua takribani, wk 2 wakatoa mfano wa 2005, jimbo la ubungo.
- Mwingine akadai, kucmama kwenye msururu mrefu, kwa muda mrefu, muda wa kuenda kutafuta chochote utatoka wapi? huyu ni yule anaye pata kipato kwa cku, asipotoka kwenda kutafuta, hapati kitu. Akahoji akitumia cku nzima akirudi atakula wapi?
- Mwingine akasema hata thithiem ikishindwa bado wata chakachua matokeo kwani bila kuongoza nchi hawana njia nyingine namna ya kuishi, hivo yeye haoni sababu ya kupoteza muda wake, kwani watafanya kila namna mpaka wapite.
TUWASHAURI JE HAWA WATU? Na wasilisha.