Wadudu waharibifu wavamia mashamba ya mahindi Babati

Wadudu waharibifu wavamia mashamba ya mahindi Babati

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
waduduuu-pic-data.jpg


Babati. Wimbi la wadudu waharibifu wa mazao maarufu kama “mbirizi” limevamia mashamba ya mahindi ya wakulima katika kata ya Kiru na vijiji vya jirani wilayani Babati mkoani Manyara.

Mkulima wa mahindi kutoka kijiji cha Kiru, Six Salao akizungumza leo Jumanne Desemba 27, 2022, amesema makundi makubwa ya mbirizi hao wanashambulia mazao ya mahindi.

Salao amesema wadudu hao ni wengi na wamejazana kwenye mashamba yao kama nzi mara baada ya msimu huu wa mvua kuanza kunyesha.

Mbunge wa zamani wa jimbo la Babati Vijijini, Vrajlal Jituson amesema wadudu hao wamevamia mashamba ya mahindi katika bonde la Kiru, hivyo wananchi wanapata hofu ya kuharibiwa kwa mazao yao.

“Wakulima wameanza kupiga dawa, hawajaisubiri serikaili ila kuna haja mamlaka husika za serikali zikajua na kuanza kutafuta mbinu za kuwatokomeza wadudu hao,” amesema Jituson.

Mkazi wa Babati, Theodora Hams amesema miaka iliyopita wazee wa eneo hilo waliwaeleza kuwa endapo wadudu hao wakivamia mashamba, ni ishara nzuri kuwa msimu huo utakuwa na mavuno mengi.

Kwa upande wake, kaimu ofisa kilimo wa mkoa wa Manyara, Samwel Dahaye amesema wadudu hao viwavijeshi vamizi waliozoea kuitwa mbirizi, hivi sasa wamejazana kwenye kata hiyo na vijiji jirani.

Dahaye amesema njia pekee ya kuwaondoa wadudu hao ni wakulima kuchukua hatua za haraka za kupiga dawa ambazo wameshauriwa na wataalamu wa pembejeo za kilimo.

“Njia nyingine ni wakulima wakague mashamba yao mara kwa mara na kuhakikisha wanaweka dawa kwenye kiini cha mche ili kuendeza ustawi,” amesema Dahaye.

Mwananchi
 
Jamani [emoji22]
Mwenye Enzi Mungu aingilie kati walahi!
 
Wasaidiwe haraka na mamlaka husika, maana hawa huwa wanakula usiku na mchana, unawezaa kuamka asubuhi shamba jeupe...
 
Hivi vidudu vinakula mpaka gunzi. Hawakuachii hata la kuwashia moto.

Ila wanadhibitika.
 
Mbirizi wanakufa ndani ya dakika 20 kama watapigwa dawa. Huu msimu funza Hawa wamemwagwa sijawahi kuona. Ila mvua zikinyesha nyingi wanakufa sana. Wanakula zaidi usiku
 
Back
Top Bottom